A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, May 29, 2018

Neymar asema yuko fiti kucheza fainali za Kombe la Dunia


Mshambuliaji nyota wa Brazil, Neymar Jr amesema yuko fiti kucheza fainali za Kombe la Dunia zinazotarajiwa kuanza Juni 14 nchini Russia bila kikwazo chochote.

Neymar ametoa kauli hiyo muda mfupi, baada ya timu hiyo kuweka kambi jijini London Uingereza kujiandaa kwa fainali hizo.

Neymar amesema ana uhakika wa kucheza mchezo wa ufunguzi dhidi ya Uswis Juni 17. “Niko tayari kucheza, hakuna kitu cha kunizuia,” alisema mchezaji huyo ambaye hajacheza muda mrefu kutokana na jeraha la kifundo cha mguu.

Hata hivyo, benchi la ufundi limejaribu kupunguza presha kwa nyota huyo kwa kuwa anahitaji muda kurejea katika kiwango bora tayari kwa fainali hizo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages