A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, May 2, 2018

Mwanaheri aelezea ishu ya kuachana na Filamu



LICHA ya madai kwamba amepigwa stop kuendelea kucheza filamu na mumewe, Khamis baada ya kuolewa hivi karibuni, mrembo wa filamu za Kibongo, Mwanaheri Ahmed ‘Mwana’ ameibuka na kueleza ukweli.

Za Motomoto News ilizungumza na Mwana ambaye alifunguka kuwa, amekuwa akiyasikia madai hayo, lakini ukweli ni kwamba hata iweje, kamwe hawezi kuachana na kazi yake ya filamu kwani ni fani anayoipenda licha ya kuwa ana elimu kubwa, lakini aliachana na kuajiriwa na kufanya kile alichokuwa anakipenda na mumewe anaheshimu hilo.

“Mume wangu anaiheshimu na anaipenda sana kazi yangu hivyo hawezi kunizuia kuigiza, bado ninaendelea na sanaa kama kawaida maana ndoa hainizuii chochote,” alisema Mwana.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages