A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, May 14, 2018

MABOSI WAVAMIA MAZOEZI YANGA, WAWAMWAGIA NOTI WACHEZAJI

KATIKA kuhakikisha wanaongeza hamasa ya timu kuelekea mechi ya pili ya hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika, mabosi wa Yanga walivamia mazoezi ya timu hiyo na kumwaga noti kwa wachezaji.


Yanga keshokutwa Juma­tano inatarajiwa kuwakari­bisha wapinzani wao Rayon Sports ya Rwandakatika mchezo huo wa makundi utakaopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Yanga tayari imepoteza mchezo wa kwanza katika kundi lao kwa kufungwa na USM Alger ya Algeriakwa kufungwa ugenini mabao 4-0.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Champi­oni Jumatatu, mabosi hao walifika katika mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika juzi kwenye Uwanja wa Chuo cha Polisi, Kurasini jijini Dar es Salaam yakiongozwa na Mkongoman, Zahera Mwinyi.

Mtoa taarifa huyo al­isema mara baada ya kufika mazoezini, mabosi hao walionekana kufuatilia kwa makini na baada ya kumalizika walipata nafasi ya kuzungumza na viongozi, benchi na kikubwa kuwapa hamasa ya mchezo ujao dhidi ya Rayon na badaye kila mchezaji na kiongozi wa benchi la ufundi alipewa shilingi 50,000.

“Leo tulipata ugenini wa ghafla wa viongozi kutoka kamati ya mashindano wakiongozwa na mwenyekiti wake Nyika (Hussein), Luku­mayi (Samuel) na kiongozi mmoja jina lake siri ambaye yeye ndiye aliyetoa fedha hizo.

“Fedha hizo zilitolewa baada ya mazoezi kumal­izika na viongozi hao kuzun­gumza machache, kikubwa wamesisitiza umuhimu wa mechi licha ya timu kukabil­iwa na matatizo ya kifedha,” alisema mtoa taarifa huyo.

Aidha, Championi Ju­matatu lilimtafuta kocha Zahera kuzungumzia hilo, akasema: “Ninafurahi kuo­na hamasa kubwa ikitolewa kwa wachezaji wangu katika kuelekea mechi na Rayon.

“Kama nilivyokwambia awali, bado baadhi ya wachezaji wameonekana kuweka mgomo kutokana na madai yao ya misha­hara, lakini nafarijika kuwaona wengine wakifika mazoezini.”
Wilbert Molandi, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages