A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, May 28, 2018

KIJANA KUTOKA MOROGORO AIWAKILISHA VEMA TANZANIA AIBUKA MSHINDI MASHINDANO YA KUSOMA NA KUHIFADHI KURUAN AFRIKA.


FANALI za Mashindano  makubwa  ya 19  ya Kusoma na Kuhifadhi Kuruan Tukufu Afrika  zimetikisa dunia ambapo  ambapo Rais Dk. John Magufuli jana amelazimika kumpigia simu Waziri Mkuu Kassim,  Majaliwa  kutaka mwakani aweze kuhudhuria fainali hizo.

Akihutubia maelfu ya watu ndani ya Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, jana, Waziri Mkuu Majaliwa alisema, akiwa uwanjani hapo, Rais Dk. Magufuli alimpigia simu na kumuuliza masuala mbalimbali kuhusu  mashindano hayo.

"Wakati niko hapa mbele nimepokea simu kutoka kwa Rais Dk. Magufuli akaniuliza hao wote walio jaa uwanja ni waislam? Nikamwambia ndiyo ila naamini kuna ambao si waislaam pia.Akauli za tena nawewe ni  mgenirasmi miaka miwili mfululizo? Nika sema ndiyo, akasema  mwakani mimi nitakuwa mgeni,”alisema Majaliwa  taarifa ilyoamsha shangwe kubwa uwanjani hapo.

Mbali na suala hilo Majaliwa alisema,   kutokana na kufana kwa mashindano hayo ambayo huandaliwa na Taasisi ya Al-Hikma Foundation ya jijini Dar es Salaam, Waziri wa Dini wa Saud Arabia  ambaye alikuwa ni mgeni mwarikwa Dk.  Saleh Mohammed Abdul Azizi Al Sheikh , ameahidi kujenga Chuo Kikuu cha Kiislamu hapa nchini.

“Waziri  wa Dini wa Saudi Arabia  amevutiwa na fainali hizi hivyo ameahidi kutujengea chuo kikuu cha kiislamu hapa nchini,”alisema Majaliwa.

Alisema, pia Waziri huyo ameahidi  mwakani atamleta Imamu  wa Msikiti wa Macca kushuhudia fainali hizo  hivyo katika fainali hizo imamu huyo atakuwa pamoja na Rais Dk. Magufuli.

“Yaani mpaka ninarengwarengwa na machozi ya furaha  kuonyesha ni namna gani mashindano haya  yanavyoliletea sifa taifa letu.Kitendo cha rais  kukubari kuhudhuria mwakani inatupa faraja kubwa,”alisema Majaliwa.

Katika hotuba yake, Waziri Mkuu  Majaliwa alizitaka taasisi za dini kuunga mkono juhudi za serikali katika kuendeleza elimu nchini.

“Ni vema kila  mmoja kuwekeza kwenye elimu.Hatuwezi  kufikia malengo  bila kuwekeza katika elimu.

Rai yangu ni kwa taasisi za dini kuendelea kuunga mkono jitihada za serikali kwa  kujenga shule na vituo vya elimu ili tuweze kuifikisha nchi yetu katika uchumi wa kati,”alisema Majaliwa.

Alisema,  serikali inatambua na kuthamini mchango wa taasisiza kidini  na itaendelea kutoa ushirikiano kwa taasisi hizo.
Pia, Majaliwa aliwataka watanzania kutunza amani  iliyopo na kuona viongozi wa dini  kujiepusha  na kauli zinazoweza kusababisha uhasama.

“Mtakubaliana nami kuwa amani ya nchi yetu, ndiyo inatufanya tutembee vifua mbele dhidi ya wenzetu, ni neema kubwa ambayo kila muumini anapaswa kuilinda kwani ikipotea hata mkusanyiko wetu huu wa leo si rahisi kufanyika mahali kama hapa,” alisema.

 Aliongeza; “Tuko hapa  kwa sababu tuna amani, kama Serikali isingekuwa inashirikisha Watanzania wote kulinda amani, basi tusingeweza kukutanika hapa. Kuna nchi 18 ziko hapa, na watu wake wamekuja hapa uwanjani kwa kuwa wana uhakika na amani tuliyonayo sisi Watanzania,” alisema.

Waziri Mkuu  Majaliwa alibainisha , nchi ambazo amani imetoweka, watu wanalazimika kufanya shughuli za ibada majumbani au kwa kujificha.

 “Wenzetu hao, hawapati fursa adhimu kama hii ya kujumuika pamoja na majirani, ndugu, jamaa na marafiki kusikiliza na kufurahia kisomo chakuruan au kufanya shughuli nyingine za kiuchumi na kijamii,” aliongeza.

 Aliwataka Watanzania waendelee kubeza na kupuuza kauli za walio wachache ambao kwao kuzungumzia amani ni kujipendekeza kwa Serikali.

“Watu hao wamesahau kwamba tofauti katika Uislamu hazikuanza leo, lakini tofauti hizo hazikuwa sababu ya wema waliotangulia kuacha kuheshimiana na kushirikiana,” alisisitiza.
Katika mashindano hayo  kijana  wa Kitanzania, Shujaa  Suleiman (23) ameibuka kidedea na kitita cha sh. milioni 15  kwenye kundi la washiriki wa juzuu 30.

Shujaa mkazi wa Morogoro, amejishindia pia kompyuta mpakato  ambapo kampuni ya City Property  Internationala Limited  imeahidi kumpa  kiwanja chenye hati eneo la Kigamboni , jijini Dar es Salaam .




 Mshindi wa pili kwenye kundi hilo la juzuu 30 ni Ahmed Noor wa Sudan ambaye ameshinda sh. Miliini 12.5 na kopmpyuta mpakato  akifuatiwa na Muzamil Awadh Mohamed wa Sudan alijishindia sh. milion 7.5 pamoja na lkompyuta mpakato.

 Mshindi wa nne ni Abdulally  Mohammed wa Kenya aliyepata zawadi ya sh. Milioni  5.7na wa tano ni Ibrahim Maazur kutoka Niger, aliyepata sh. Milioni 3.4.

 Washindi hao wote watano walipewa zawadi ya kwenda hijja na Waziri wa Mambo ya Dini wa Saudi Arabia, Dk. Saleh Ally Sheikh.

 Washiriki wengine kwenye kundi la juzuu 30 walitoka nchi za Rwanda, Burundi, Msumbiji Djibouti, Kenya, Ethiopia, Congo DRC, Nigeria, Ghana na Afrika Kusini.
Washiriki wengine waliopewa zawadi ni wale walioweza kuhifadhi Juzuu tatu (washindi watatu), Juzuu tano (washindi watatu); Juzuu 10 (washindi watatu) na Juzuu 20 (washindi watatu).

 Viongozi wengine waliohudhuria mashindano hayo ni Makamu wa Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dk. Mohammed Gharib Billal, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania kutoka Saudi Arabia, Comoro, Oman, Uturuki, Kenya, Msumbiji na Nigeria, Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir bin Ally na Rais wa taasisi ya Al-Hikma, Sheikh Sharif Abdilkadir Al-Ahdal.
   
 Waziri Mkuu amemtaka Sheikh Nurdin Mohammed Ahmad (maarufu kama Sheikh Kishki) akaonane na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bw. William Lukuvi ili atoe maamuzi ya kiwanja chao kilichopo eneo la Matumbi ambacho mwaka jana aliagiza kifuatiliwe taratibu zake na kisha wapatiwe.

“Kuhusiana na suala la kiwanja mlichosema, mamlaka ya awali ni Manispaa ya Temeke na ilishakamilisha taratibu zote za kisheria, ikapeleka kwa Afisa Ardhi wa Mkoa kuona kama limepita kwenye vikao vyote ndipo wanaenda wizarani kupata kibali. Hakuna sababu ya wizara kuikatalia manispaa huku eneo lenyewe likiwa kwenye ramani kuu ya manispaa yenyewe, nenda mumuone Waziri mwenye dhamana, awape ardhi,” alisema.

Waziri Mkuu amefikia hatua hiyo baada ya kupewa taarifa akiwa jukwaani kwamba taasisi ya Al-Hikma iliwasiliana na Manispaa ya Temeke, hadi mkoani wakapewa barua zinaonyesha eneo liko sawa lakini walipofika wizarani wamekwamishwa na Afisa mmoja aliyemtaja kwa jina moja la Mama Mpetula.

Juni 11, mwaka jana katika mashindanio ya 18, taasisi ya Al-Hikma waliomba wapatiwe kiwanja na.118 kwenye kitalu E kilichoshikamana na kiwanja na. 117 chenye shule yao ya Al-Hikma Girls iliyoko Temeke ili waweze kujenga zahana.

 Matukio katika picha
























No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages