Video queen maarufu nchini, Agnes Gerald ‘Masogange’ amefariki dunia hivi punde (leo Aprili 20, 2018) katika Hospitali ya Mama Ngoma, Mwenge jijini Dar es Salaam baada kuzidiwa ghafla jana na kukimbizwa hospitalini hapo.
Taarifa ambazo hazijathibitishwa, zinadai Masogange alifikishwa Hospitalini hapo akisumbuliwa na homa ya matumbo na tatizo la kupungukiwa na damu.
Dkt. Kihama Ngoma ameithibitishia Global Publishers na kusema taarifa zaidi zitatolewa baadaye.
Taarifa zaidi tutakueletea hapa hapa.
huo.
No comments:
Post a Comment