A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, January 25, 2018

RC MAKONDA LICHA YA KUMTUKANA RAIS MAGUFULI BADO SERIKALI INA MAPENZI NA WANANCHI WAKE



Jengo hilo la kisasa lenye Gorofa Moja limepewa jina la HON. PAUL MAKONDA OBSTETRIC THEATRE Kama sehemu ya kuenzi jitiada za RC Makonda kuboresha Sekta ya Afya kwa kumtafuta mfadhili GSM Foundation aliekubali kujenga Jengo hilo bila kutumia pesa ya Serikali. 




RC Makonda aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo hilo mnamo March 13 siku ambayo ndio aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa na sasa jengo limekamilika likiwa na Vyumba Viwili vya Upasuaji vyenye uwezo wa kufanya upasuaji kwa wakati mmoja na kuhudumia Wagonjwa 20 kwa siku.

RC Makonda amesema kabla ya kujengwa kwa jengo hilo Wagonjwa walikuwa wakisongamana kusubiri kufanyiwa upasuaji kitendo kilichokuwa kikisababisha Maumivu Makali na Vifo vya Mama na Mtoto lakini kupitia jengo hilo vifo vinaenda kupungua. 


Makonda ameishukuru GSM Foundation kwa kufanikisha Ujenzi wa Jengo hilo ambapo inakadiriwa Hospital ya Mwananyamala inapokea Wagonjwa kuanzia 1,500 hadi 2,000 kwa siku na Kati ya hao ni Wajawazito wanaohitaji huduma ya Upasuaji.







 RC Makonda amesema hadi sasa zaidi ya Kinamama 55 wamejifungua salama ndani ya jengo hilo na linaendelea kupokea kinamama Wajawazito kila kukicha. 

 PICHA MBALIMBALI ZIKIMUONESHA  RC MAKONDA KATIKA JENGO JIPYA KA UPASUAJI KWA WAMAMA WAJAWAZITOWAJAWAZITO



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages