A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, November 7, 2017

Vijana wa timu ya Argexas ya Buguruni wamkosha Mbunge Anatropia Theonest.


MBUNGE wa Viti Maalum katika Manispaa ya Ilala kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Anatropia Theonest alieshika kombe kabla yakuwakabidhi washindi wa mashindano hayo
Kinyerezi Fc Wakipokea zawadi baada yakuibuka mshindi wa pili katika mashindano ha
Baadhi ya mashabiki wakimshukuru Mbunge wa Viti Maalum katika Manispaa ya Ilala kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Anatropia Theonest. kwakuandaa mashindano hayo.
Mmoja wa viongozi wa mashindano hayo akiongea jambo na washiriki mapoja na mashabiki wa mchezo huo.

MBUNGE wa Viti Maalum katika Manispaa ya Ilala kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Anatropia Theonest ameahidi kudhamini timu ya vijana ya Argexas ya Buguruni jijini Dar es Salaam hadi kuiwezesha kufikia Ligi Kuu.


Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi baada ya kumalizika kwa fainali ya mashindano ya Kombe la Anatropia Segerea ambayo yeye ndio muandaaji wake, Anatropia alisema amelazimika kuandaa mashindano hayo ili kuwaweka karibu vijana na kwamba  timu ya Argexas iliyoibuka na ubingwa ataifadhili ili kuiwezesha kufika mbali hadi kucheza ligi kuu.


Alisema sambamba na kuisaidia pia atakuwa akiibua vijana  mbalimbali wenye vipaji ambao watakuwa wakiongeza nguvu katika timu hiyo ambayo anaamini itafika mbali kutokana na uwezo mkubwa walioonyesha.


“Natamani hii timu ije iwe timu bora katika Manispaa ya Ilala na pia nitafurahi zaidi pale nitakapoona inafika kucheza katika ligi kuu,” alisema Anatropia.


Alisema anatarajia kuyafanya mashindano hayo kuwa ya muendelezo ili kuweza kutimiza lengo la kuwaweka karibu vijana ikiwa ni pamoja na lile la kupinga unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya watoto katika Manispaa ya Ilala ifikapo 2020.


Alisema hadi kufika hatua ya fainali, mashindano hayo yalishirikisha timu 24 na kwamba mshindi wa kwanza alizawadiwa ng’ombe, kombe, jezi na mpira mmoja huku mshindi wa pili akipata mbuzi wawili, jezi na mpira mmoja.


Aliongeza kuwa mshindi wa tatu alipata jezi na mpira mmoja huku mfungaji bora kutoka katika timu ya Argexas ambayo ndio bingwa wa mashindano alimzawadia pesa taslimu sh 100,000. 

Mwisho.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages