A great place to access the latest news and information.

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, November 10, 2017

SERIKALI KUPUNGUZA MIMBA ZA UTOTONI

Mkurugenzi Mtendaji wa Jukwaa la Utu wa Mtoto wa Kike (CDF) Koshuma Mtengeti, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam

SERIKALI imejipanga kupunguza mimba za utotoni  kwa asilimia 27 kwa kipindi cha  miaka mitano kinachoanzia  2017 hadi 2022 lengo likiwa ni kuhakikisha mototo wa kike anapata haki yake ya elimu.

Hayo yamesema leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Maendeleo ma watoto kutoka Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii jinsia na Watoto, Margareth Mussai wakati Kongamano la Mtoto wa Kike , liloandaliwa na Jukwaa la  Utu wa Mtoto wa Kike (CDF) kwa udhamini wa Shirika la Maendeleo  Uswidi ( Swedish International Development Cooperative Agency-SIDA).

Mussai amesema kwa sasa serikali imeandaa mpango kazi wa Taifa wa kotokomeza ukatili wa kijinsi kwa upande  Mimba za Utoto.

“Katika Mpango  huu tumeanza kupunguza mimba kwa asilimia 27 kwa watoto na tunaamini mpango huu utasaidia kundokana na tatizo hili”Amesema

Amesema katika kutekeleza mpango huu, Serikali  itashirikiana Taasisi zisizo za Kiserikali  katika kuhakikisha wanapunguza Mimba za Watoto.

Hata hivyo , Mussai amewataka Watoto wa Kike  kujitambua wenyewe kwa kujiepesha na mambo yasio faa ambayo yatapelekea kuongezeka mimba za watoto ambapo amedai zimechangiwa na watoto hao kujiingiza kwenye makundi yasioa faa.

Kw upande wake Mkurugenzi wa Mtendaji wa CDF Koshuma Mtengeti, amesema lengo la kongamano hilo ni kuwapatia fursa watoto wa kike kukurana na Mkurugenzi Mwandamizi wa Shirika la Uswid  ambapo watapata fursa ya kuelezea mafunzo mbali mbali waliyopata kutokana na utekelezaji wa miradi mbali mbali ya CDF.

Amesema miradi hiyo ni pamoja na miradi ya kutokomeza, mimba za utotoni, ndoa za utotoni, ukatili wa kijinsia na kuonesha kazi za ujasiriamali walizozifanya ikiwa kama mafanikio ya miradi ya CDF.

“Vile vile katika kongamano hili, wanaume na wavulana wakiwa kama mabalozi wa CDF watapata fursa ya kuelezea ni kwa namna gani wanafanya kazi za kuelimisha jamii pamoja na vijana rika juu ya madhara ya ukatili wa kijinsia, ukeketaji, mimba za utotoni pamoja na ndoa za utotoni ili kufikia dhana ya Taifa ya kuleta usawa wa kiiinsia,” amesema Mtengeti.

Mkurugenzi Mwandamizi kutoka SIDA Carin Jamtin, amesema shirika lao limekuwa likitetea haki za woto kwa kuhakikisha watoto wakike na kiume wanakuwa na haki sawa katika jamii hususani haki ya kupata elimu.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages