A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, November 7, 2017

ARGEXAS YA BUGURUNI YAIBUKA KIDEDEA MASHINDANO YA ANATROPIA CUP 2017




TIMU ya soka ya Argexas juzi imeibuka bingwa wa mashindano ya kombe la Segerea 2017 baada ya kuichapa timu ya Kinyerezi Fc mabao 2-0 katika mchezo uliofanyika katika uwanja ya Toto Tundu uliopo Tabata Segerea jijini Dar es Salaam.

Mashindano hayo yaliyoandaliwa na Mbunge wa Viti maalum katika Halmashauri ya Ilala kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) , Anatropia Theonest yalishirikisha timu 24 za vijana.

Katika mchezo huo wa fainali uliochezwa huku mvua kubwa ikinyesha, timu ya Argexas ilionekana kutawala mchezo katika kipindi chote cha kwanza huku ikikosa magoli mengi ya wazi.

Hata hivyo katika dakika ya 46 ya kipindi cha kwanza kupitia kwa mchezaji Rashid Ismail, timu ya Argexas iliweza kupata bao lake la kwanza kabla ya dakika ya pili baadae kupitia kwa Patrick Muhagama aliyepiga shuti kali lililomfanya kipa wa Kinyerezi abaki ameshika kichwa asiamini macho yake.

Baada ya mpambano huo kumalizika, mshindi wa kwanza alikabidhiwa zawadi ya Ngombe, kikombe, jezi pamoja na mpira mmoja huku mshindi wa pili ambaye ni Kinyerezi Fc alipata Mbuzi wawili, jezi pamoja na mpira mmoja.

Timu ya Tabata Future ambayo ilishika nafasi ya tatu ilipata jezi pamoja na mpira mmoja huku mfungaji bora wa mashindano kutoka katika timu ya Argexas Rashid Ismaili alizawadiwa na muandaaji wa mashindano pesa tasilimu sh 100,000.

Akizungumza baada ya kukabidhi zawadi, Anatropia alisema mashindano hayo yatakuwa endelevu na kwamba lengo ni kuwaweka karibu vijana pamoja na kuendesha kamapeni ya vunja ukimywa yenye lengo la kuondoa unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya watoto katika manispaa ya Ilala.

Alisema mashindano hayo yalianza kutimua vumbi miezi miwili iliyopita na kwamba timu 24 zilishiriki ambapo baada ya mzunguko wa kwanza kumalizika zilibaki timu 16 ambazo kati ya hizo nane zilifika hatua ya robo fainali na baadae nne zikacheza hatua ya nusu fainali iliyowezesha kufikia fainali kwa kuzikutanisha timu za Kinyerezi Fc na Argexas.


Mbunge wa Viti maalum katika Halmashauri ya Ilala kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) , Anatropia Theonest  akimkabidhi zawadi mfungaji bora kutoka katika timu ya Argexas ambayo ndio bingwa wa mashindano alimzawadia pesa taslimu sh 100,000. 


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages