Baadhi
ya Wazee wa kata ya Manzese wakisubiri huduma ya Usajili katika zoezi
la kuwasajili wazee linaloendelea Wilayani humo kwa kuratibiwa na
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa ofisi ya Wilaya ya Ubungo.
Zoezi
la kuwasajili Wazee Kata ya Manzese likiendelea.Katika picha ni mmoja wa
wananchi akisubiri kupigwa picha katika moja wapo ya hatia za Usajili
na uchukuaji alama za Kibaiolojia.
Ndg.
Anthony Mwasiguhu Afisa usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa
akiingiz taarifa za Bi. Fatuma kwenye mfumo wa Usajili wakati zoezi la
kuwasajili wazee likiendelea Kata ya Manzese.
Bi.
Neema Mbila Afisa Usajili Wilaya ya Ubungo akimsaidia Bi.Fatuma
kujisajili wakati wa hatua ya uchukuaji alama za vidole, picha na saini
ya kielektroniki wakati wazoezi la kuwasajili wazee linaloendelea
sambamba na usajili wa kadi za Afya kwa Wilaya ya Ubungo.
Wazee
wa Kata ya Manzese Wilaya ya Ubungo mkoa wa Dar-es-Salaam wamefurahishwa
na kitendo cha serikali kupitia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa(NIDA)
kuwapatia fursa maalumu ya kusajiliwa Vitambulisho vya Taifa na wao
kutambulika kama Raia sambamba na zoezi linaloendelea sasa la kuwasajili
Kadi za Afya mpango ulio chini ya Manispaa ya Ubungo.
Wakizungumza
wakati wa Usajili unaoendelea katika kata hiyo ukihusisha ujazaji fomu
za maombi ya Vitambulisho, uchukuaji alama za Vidole, picha na Saini za
Kielektroniki; wazee hao wamesema hii kwao imekuwa ni fursa ya pekee na
kuomba NIDA kuendelea kusogeza huduma hizi kwa wazee waliopo kwenye
maeneo mengine nchini.
Mzee
Sudi Abdallah Sudi amesema “ Hii ni fursa adhimu sana na tunaomba
muendee na moyo huu wa kutujali wazee na kusogeza huduma hii kwa wazee
waliopo kwenye Kata zingine kwani itawasaidia wazee. Wazee wengi
tunakosa fursa nyingi zikiwemo huduma mbalimbali kutokana na umri wetu
mkubwa kwa kushindwa kutembea umbali mrefu kufuata huduma zilikowekwa”
Kwa
mujibu wa Afisa Usajili wilaya ya Ubungo (DRO) Ndugu Abdulrahman Muya
ameeleza kuwa NIDA kwa kushirikiana na Manispaa ya Ubungo imefanikiwa
mpaka sasa kusajiliwa wazee 500 katika awamu ya kwanza ya Usajili na
wataendelea na awamu ya pili lengo likiwa kukamilisha Usajili wa wazee
wote wanaoishi katika Wilaya hiyo.
Zoezi
la Usajili Vitambulisho vya Taifa mbali na kuendelea katika Ofisi zote
za Wilaya katika Mkoa wa Dar-es-salaam, zoezi hilo kwasasa linaendelea
nchi nzima kupitia ofisi za NIDA zilizofunguliwa kwenye kila Wilaya nchi
nzima.
No comments:
Post a Comment