Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda leo anawatangazia
Wafanyabiashara Wote wa Viwanda Vidogovidogo Dar es Salaam kufika Ofisi
ya Mkuu wa Mkoa kupatiwe Mkopo wenye Riba Nafuu ili kukuza Biashara zao
kufikia kiwango cha Kati kisha kuwa na Viwanda Vikubwa.
Hatua
hiyo ni baada ya Makonda kufanya mazungumzo jana na Mfuko wa hifadhi
ya Jamii NSSF kuhusu kuwekeza Wafanyabiashara wadogo Mkoa wa Dar es
salaam ambao baada ya mazungumzo hayo NSSF imemkubalia kutoa fedha za
kutosha kwaajili ya kuwakopesha wenye Viwanda Vidogovidogo.
Kwa
mantiki hiyo Makonda amewataka Wafanyabiashara hao kufika Ofisi ya Mkuu
wa Mkoa na kuonana na Afisa Biashara wakiwa na Mchanganuo wa Biashara
zao kisha kueleza kiwango cha Fedha wanazotaka kukuza Biashara zao na
kuongeza uzalishaji.
Mheshimiwa
Makonda amesema lengo la Mpango huo ni kuwawezesha Wafanyabiashara kuwa
na Mitaji itakayowafanya kukuza Viwanda vyao ili kufikia malengo na
azma ya Rais Dr.John Magufuli ya kuwa na Tanzania ya Viwanda.
Katika
juhudi za kuwakwamua Wafanyabiashara wazawa Makonda ameeleza mpango wa
kuanzisha Soko la kuonyesha na kuuza bidhaa zinazozalishwa na wazawa
kila Mwezi mara Moja kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja.
Aidha
Makonda amezielekeza Manispaa zote za Mkoa wa Dar es Salaam kuhakikisha
10% ya fedha zinazotengwa kwaajili ya kuwakopesha Kinamama, Vijana na
Walemavu zinatolewa kwa Wafanyabiashara wenye Viwanda Vidogovidogo ili
kuwaongezea nguvu.
Katika
hatua nyingine Makonda amewataka Wamachinga kutoa kipaombele kwa kuuza
Bidhaa zinazozalishwa na Wafanyabiashara wazawa ilikukuza uchumi wa
Tanzania.
Post Top Ad
Your Ad Spot
Wednesday, September 27, 2017
RC MAKONDA SASA KUTOA MIKOPO YA RIBA NAFUU KWA WAJASIRIAMALI WOTE DAR ES SALAAM
Tags
KITAIFA#
Share This
About kilole mzee
KITAIFA
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment