A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, August 10, 2017

TEF WAONDOA ZUIO LA KUTOKUTOA HABARI ZA MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM, MAKONDA

JUKWAA la wahariri Tanzania (TEF) laondoa zuio la kutokutoa habari za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Mkonda jijini Dar es Salaam. 

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Theophil Makunga amesema kuwa " Mgogoro huu kati ya Jukwaa la wahariri wa habari na tasnia ya habari  na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Mkonda umefika mwisho tunarusu sasa habari zake ziandikwa  mgogoro ule uliokuwepo yaliyopita si ndwele tugange yajayo"

Tamko hilo la TEF limekuja mara baada ya Machi 22 mwaka huu kutoa tamko lao kwa vyombo vya habari  lililokuwa likisema "Zinalaani vikali vitendo vya Mkuu wa Mkoa katika kuvamia chombo cha habari cha Clouds Media akiwa ameambatana na Askari wenye silaha.

Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la wahariri Tanzania(TEF), Deodatus Balile (katikati) akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.  Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na Mkurugenzi wa Vipindi na uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Theophil Makunga akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari jijini Dar es Salaam kwaajili ya kuondoa adhabu aliyopewa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ambayo alikua nayo ikiwa Jukwaa hilo la wahariri lilimfungia kwa  kutokutoa habari yoyote kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Vipindi na uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda wa pili (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana. wakati Jukwaa la wahariri Tanzania (TEF) wakiondoa zuio la kutokutoa habari yoyote kwenye chanzo cha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwenye vyombo vya habari  sasa kuanzia leo habari za mkuu wa Mkoa  zitakuwa zikitoka kwenye vyombo vyote vya habari. (kushoto) ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Theophil Makunga, Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la wahariri Tanzania(TEF), Deodatus Balile, na Mkurugenzi wa Vipindi na uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba.   
Mkurugenzi wa Vipindi na uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba (kushoto)akizungumza na waandishi wa  habari jijini Dar es Salaam kwenye hafla hiyo.
Baadhi ya waandishi wa habari na wahariri waliohudhulia Mkutano wa Jukwaa la wahariri Tanzania (TEF),

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages