MGOMBEA wa nafasi ya Makamu wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Mulamu Nghambi, leo amezindua kampeni zake rasmi na kutaja vipaumbele vitano atakavyofanyia kazi iwapo atachaguliwa katika nafasi hiyo.
Nghambi ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Dodoma (Dorefa)anawania nafasi hiyo katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Agosti 12, mwaka huu mkoani Dodoma.
Katika
uzinduzi alioufanya leo jijini Dar, Nghambi ambaye amekuwa kiongozi wa
soka kwa miaka 18, alisema kuwa moja ya vitu atakavyohakikisha vinakuwa
sawa ni suala la ushirikiano na viongozi wengi kwa lengo la kuleta
maendeleo ya mchezo huo nchini.
“Endapo
nitapa nafasi hii ambayo nawania katika uchaguzi, naahidi kuwa
nitaitendea haki kutokana na uzoefu nilio nao kwa kutumikia soka katika
nyadhifa mbalimbali kwa kipindi cha miaka 18 sasa".Alisema
“Dhamira kubwa si kuongelea uzoefu wangu ila kuweka wazi malengo yangu ya
msingi yaliyonisukuma kuwania nafasi hii na ushirikiano na viongozi
wenzangu, mipango ya muda mfupi na muda mrefu ambayo naamini itakuwa na
faida kubwa katika kukuza soka letu,” alisema Nghambi.
No comments:
Post a Comment