A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, March 9, 2022

SPORTPESA YAJA NA PROMOSHENI MPYA YA BET BONANZA.

 

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KAMPUNI ya Michezo ya Kubashiri nchini ya Sportpesa imezindua promosheni mpya ya Bet Bonanza kwa lengo la kutoa pesa zaidi kila siku kwa Wateja wake sambamba na wachezaji wengine wa michezo ya kubashiri kupitia mitandao ya Vodacom (M-Pesa) na Artel (Airtel Money).

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni hiyo, Tarimba Abbas amesema amesema Promosheni hiyo imeanza Machi 8, 2022 ambapo washindi wa Promosheni hiyo watazawadiwa Shilingi Elfu Ishirini (Tsh. 20,000/-) kwa kila siku, kwa washindi kumi kutoka Airtel Money na M-Pesa.

Tarimba amesema Promosheni hiyo itadumu kwa siku 35 hadi Aprili 12, 2022, sambamba na zawadi za kila siku pia, kutakuwa na zawadi za kila wiki ambayo ni Shilingi Milioni Moja (Tsh. 1,000,000), amesema mwisho wa Promosheni, mshindi atapata zaidi ya Shilingi Milioni 15 (Tsh. 15,888,000).

Tarimba amesema Promosheni hiyo inatoa fursa kwa wachezaji wa Sportpesa kushiriki vizuri katika ubashiri wa Ligi mbalimbali duniani, na zaidi ya bashiri za kawaida ambazo zina ujazo mwingine.

Kwa upande wake, Meneja Mauzo wa M-Pesa Kelvin Nyanda amewakaribisha Wateja wa Mtandao wa Vodacom kushiriki kubashiri kwa Bet Bonanza na kujishindia Pesa zaidi kupitia Promosheni hiyo.

Naye, Meneja Biashara wa Airtel, Aggrey Charles amehimiza kushiriki Promosheni hiyo kupitia Menu ya Airtel Money ya *150*60# ili kuweza kushiriki bashiri hizo au kupitia ‘Application’ ya Airtel. Promosheni hiyo ni kwa Watumiaji waliojisajili Sportpesa, Wateja wa Vodacom na Airtel.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni y Sportpesa, Abbas Tarimba (wa pili kutoka kulia) akizungumza wakati wa utambulisho wa Promosheni ya Bet Bonanza ambayo watumiaji wake watashinda zawadi ya pesa kila siku. Wa kwanza kutoka kulia ni Meneja Biashara Airtel, Aggrey Charles, wa Tatu kutoka kulia ni Meneja Mauzo wa M-Pesa, Kelvin Nyanda.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages