Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KAMPUNI
ya Michezo ya Kubashiri nchini ya Sportpesa imezindua promosheni mpya
ya Bet Bonanza kwa lengo la kutoa pesa zaidi kila siku kwa Wateja wake
sambamba na wachezaji wengine wa michezo ya kubashiri kupitia mitandao
ya Vodacom (M-Pesa) na Artel (Airtel Money).
Akizungumza
na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi ya Kampuni hiyo, Tarimba Abbas amesema amesema Promosheni
hiyo imeanza Machi 8, 2022 ambapo washindi wa Promosheni hiyo
watazawadiwa Shilingi Elfu Ishirini (Tsh. 20,000/-) kwa kila siku, kwa
washindi kumi kutoka Airtel Money na M-Pesa.
Tarimba
amesema Promosheni hiyo itadumu kwa siku 35 hadi Aprili 12, 2022,
sambamba na zawadi za kila siku pia, kutakuwa na zawadi za kila wiki
ambayo ni Shilingi Milioni Moja (Tsh. 1,000,000), amesema mwisho wa
Promosheni, mshindi atapata zaidi ya Shilingi Milioni 15 (Tsh.
15,888,000).
Tarimba
amesema Promosheni hiyo inatoa fursa kwa wachezaji wa Sportpesa
kushiriki vizuri katika ubashiri wa Ligi mbalimbali duniani, na zaidi ya
bashiri za kawaida ambazo zina ujazo mwingine.
Kwa
upande wake, Meneja Mauzo wa M-Pesa Kelvin Nyanda amewakaribisha
Wateja wa Mtandao wa Vodacom kushiriki kubashiri kwa Bet Bonanza na
kujishindia Pesa zaidi kupitia Promosheni hiyo.
Naye,
Meneja Biashara wa Airtel, Aggrey Charles amehimiza kushiriki
Promosheni hiyo kupitia Menu ya Airtel Money ya *150*60# ili kuweza
kushiriki bashiri hizo au kupitia ‘Application’ ya Airtel. Promosheni
hiyo ni kwa Watumiaji waliojisajili Sportpesa, Wateja wa Vodacom na
Airtel.
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni y Sportpesa, Abbas Tarimba (wa pili
kutoka kulia) akizungumza wakati wa utambulisho wa Promosheni ya Bet
Bonanza ambayo watumiaji wake watashinda zawadi ya pesa kila siku. Wa
kwanza kutoka kulia ni Meneja Biashara Airtel, Aggrey Charles, wa Tatu
kutoka kulia ni Meneja Mauzo wa M-Pesa, Kelvin Nyanda.
No comments:
Post a Comment