Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na
Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Abdulmajid Nsekela pamoja na viongozi
wengine Wakuu wa CRDB pamoja na Serikali akivuta kitambaa kuashiria
ufunguzi wa Jengo la Makao Makuu ya Benki hiyo yaliyopo Palm Beach,
Mkabala na Barabara ya Ali Hassan Mwinyi Jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na
viongozi wengine Wakuu wa CRDB pamoja na Serikali akiminya kitufe
kuashiria ufunguzi wa Jengo la Makao Makuu ya Benki ya CRDB lililopo
Palm Beach, Mkabala na Barabara ya Ali Hassan Mwinyi Jijini Dar es
Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na
Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Abdulmajid Nsekela wakati akikagua Ofisi
mbalimbali za Makao Makuu ya Benki ya CRDB yaliyopo pembezoni mwa
Barabara ya Ali Hassan Mwinyi Jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu akiwa pamoja na
Wajumbe wa Bodi ya Benki ya CRDB pamoja na viongozi wengine wa Serikali
katika ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Benki ya CRDB yaliyopo
pembezoni mwa Barabara ya Ali Hassan Mwinyi Jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu akizungumza na
viongozi mbalimbali pamoja na Wafanyakazi wa CRDB mara baada ya kuzindua
jengo la Makao Makuu ya Benki ya CRDB yaliyopo pembezoni mwa Barabara
ya Ali Hassan Mwinyi Jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu akiagana na
viongozi mbalimbali wa Benki ya CRDB mara baada ya kuzungumza nao katika
viwanja vya Agha Khan Jijini Dar es Salaam.
Dar es Salaam, Tanzania | Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema
uwepo wa sekta ya kibenki iliyo imara nchini huchangia kwa kiasi kikubwa
kupunguza tatizo la ajira na kutoa fursa kwa wananchi kujiongezea
kipato.
Rais
Samia amesema hayo katika Hafla ya Uzinduzi wa Makao Makuu ya Benki ya
CRDB iliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Rais
Samia amesema benki ya CRDB imefanya vizuri katika kutoa fursa za
ajira, biashara na ujasiriamali kwa sekta binafsi wakiwemo bodaboda,
mama lishe na wamachinga.
Aidha,
Rais Samia ameitaka benki hiyo kuendelea kuyawezesha makundi hayo ili
kutayarisha walipa kodi na kutanua wigo wa Serikali kukusanya mapato
kupitia makundi hayo.
Rais
Samia pia amesema Serikali itaendelea kushirikiana na taasisi za
kifedha huku akiongeza kuwa sekta za kibenki zina jukumu la kufufua
uchumi uliodorora kutokana na UVIKO 19.
Serikali
kupitia Benki Kuu imeanzisha mpango mahsusi wa kuiwezesha sekta ya
kibenki kupata mikopo yenye riba nafuu ambapo imetenga jumla ya shilingi
Trilioni moja kwa ajili ya kuyakopesha mabenki kwa masharti nafuu
zitakazowezesha kuikopesha sekta binafsi nchini.
No comments:
Post a Comment