A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, January 19, 2022

YANGA YAICHAPA MBUNI FC MABAO 2-0, MECHI YA KIRAFIKI

 

FB_IMG_1642611449756
Na Mwandishi Wetu, Arusha | Klabu ya Yanga Sc leo imeshuka dimbani katika mechi ya kirafiki akicheza na timu ya Mbuni Fc kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha.

Kwenye mchezo huo Yanga imefanikiwa kuondoka na ushindi wa mabao 2-0, mabao yote yakiwekwa kimyani na kiungo raia wa Dr Congo Mukoko Tonombe.

Mukoko ambaye usajili wake kwenda TP Mazembe kukwama leo hii alipewa nafasi ya kucheza kwa kwa dakika 90 na kuiwezesha timu yake kuondoka na ushindi ambapo mabao yote alifunga kwa Penati.

Yanga Sc iliwapa nafasi wachezaji wake wapya na ambao hawapo katika kikosi cha kwanza ili kuweza kumshawishi kocha na kuwajumuisha kwenye kikosi cha kwanza.

Yanga Sc iliwaanzisha wachezaji Johora, Paul Godfrey,Bryson, Bacca, Mukoko, Sureboy,Ambundo,Kaseke, Faridi na Makambo

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages