A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, January 20, 2022

Gari la abiria lagonga treni jijini Dar es Salaam, wawili wafariki, sita wajeruhiwa

 UONGOZI wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) umethibitisha kutokea kwa tukio la ajali lililotokea Januari 19, 2022 maeneo ya Banana jijini Dar es Salaam katika kivuko cha reli na barabara, ambapo gari la abiria aina ya ‘Coaster’ lenye namba za usajili T701 CKD linalofanya safari kati ya Tandika na Mbezi limegonga treni.

"Ajali imetokea majira ya saa 11:10 jioni na imehusisha treni ya mjini inayotoa huduma ya usafiri wa abiria kati ya Kamata na Pugu jijini Dar es Salaam, katika ajali hii majeruhi ni abiria 6 waliokuwa wakisafiri na basi ambapo wanawake ni watatu na wanaume watatu na kuna vifo vya wanawake wawili, majeruhi wote wamepelekwa Hospitali ya Amana kupatiwa matibabu.

"Dereva wa basi alitahadharishwa kwa kupigiwa honi na dereva wa treni, hakuzingatia na hata aliposimamishwa na mshika bendera dereva wa basi aliamua kukatiza reli na kupelekea ajali.

"Uongozi wa Shirika la Reli Tanzania unaendelea kusisitiza Umma kuwa makini na kufuata Sheria na taratibu zinazoonesha alama zilizopo katika vivuko vya reli na barabara na dereva anapokaribia makutano anapaswa kupunguza mwendo na kusimama umbali wa mita 100 kuhakikisha endapo njia ni salama ili kuendelea na safari;

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages