A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, April 21, 2021

DIWANI KATA YA MSASANI AHAHA KUWANUSURU WANANCHI WAKE ADHA YA MAFURIKO


Diwani wa Kata ya Msasani,Kionondoni, Jijini Dar es Salaam,Luca Neghesti, akikagua mifereji anayoijenga kwa nguvu zake binafsi   ili kuwaondolea adha ya muda mrefu ya mafuriko  wananchi, Dar es Salaam, leo.


WANANCHI wa Kata ya Msasani,Kionondoni, Jijini Dar es Salaam, wamempongeza Diwani wa Kata hiyo Luca Neghesti kwa jitihada binafsi anazofanya za kujenga mitaro  ya kupitishia maji ya mvua  ili kuwaondolea adha ya muda mrefu ya mafuriko wakati wa masika.

Wananchi hao walisema kwa miaka mingi kata hiyo ilikuwa ikikabiliwa na adha kubwa ya mafuriko kutokana na barabara za mitaa kutokuwa na mifereji hivyo kusababisha adha kwa wananchi.

Wakizungumza  leo , wananchi hao walisema hatua ya Diwani  Luca kuanza kujenga mifereji hiyo kwa nguvu yake binafsi ni  kutambua  haki za wanyonge  jambo ambalo lilitiwa mkazo na Hayati Rais Dk. John Magufuli na kuomba aungwe mkono na serikali, taasisi, wadau  na mashirika ili kukabiliana na changamoto hiyo.

“Kata ya Msasani tumeteseka kwa miaka mingi na adha ya mafuriko. Hakuna uongozi uliotukumbuka. Tunamshukuru Diwani Luca ameanza kuthubutu  kutatua kero hii. Kikubwa tunaomba Halmashauri ya Manisapaa ya Kinondoni , serikali, taasisi  wadau na mashirika kumsaidia hata kifusi tu,”anasema Barnabas Modest Mkazi wa  Mtaa wa Mikoroshini.

Kapilima Ismail, alisema kwa miaka mingi wananchi katika eneo hilo wamelalamika  kuhusu adha kubwa ya mafuriko kutokana na barabara kuto kuwa na mitaro  lakini hawakusikilizwa.

“Diwani Luca tumeanza kuona jitihada zake japo kwa muda mfupi wa uongozi wake. Tunaamini  kama ataongezewa nguvu basi Kata ya Msasani itarudi katika hadhi yake ,”amesema.

Leila Kibwana aliema,  Diwani Luca anatoa tumaini kubwa kwa wananchi wa kata hiyo ambao mvua inaponyesha nyumba huzingirwa na maji na katika maeneo mengine maji huingia ndani na kuleta adha kubwa.

“Tunaomba aungwe mkono hata kwa kifusi.Ameonyesha njia na mwelekeo kwa kujenga mifereji hii kwa nguvu zake mwenyewe, hii inatokana na imani kubwa aliyonayo kwetu sisi wananchi wanyonge. Tunaomba  wadau wamsaidie kukamilisha kazi hii.

Wananchi hao walise utekelezaji wa Ilani ya CCM si kwa miradi mikubwa tu bali pia midogo lakini inayo gusa maisha ya wanyonge kama anavyo tekeleza diwani wao  huyo.

Kwa upande wake Diwani Luca (CCM), alisema  ameanza ujezi wa mitaro  kwa nguvu zake mwenyewe  baada  katika mitaa ya Kata hiyo ili kuwanusuru wananchi wake kwa  adha ni kubwa  wanayo pata  katika kipindi cha mvua ambapo maji hutapakaa mitaani na hata kuingia ndani ya nyumba.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages