A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, July 23, 2020

Trump kutuma wanajeshi katika miji yenye ghasia


Rais Donald Trump wa Marekani ametangaza kwamba atatuma maafisa wa kijeshi kwenye miji ya Chicago na Albuquerque katika jimbo la New Mexico kusaidia kukabiliana na ongezeko la matukio ya kihalifu, hatua inayozidisha uingiliaji kati wa serikali kuu kwenye serikali za majimbo katika kipindi ambacho anawania kurejea tena madarakani akitumia kauli mbiu ya amani na sheria.

 Trump amesema katika siku za hivi karibuni kumekuwapo na vuguvugu la mrengo mkali wa kushoto ambalo linapigania kupunguza kiwango cha bajeti inayotengewa idara ya polisi, kuinyanganya silaha na hata kuivunjilia mbali idara hiyo.

Wataalamu wa masuala ya sheria za jinai wanasema, hata hivyo, maelezo haya ya Trump kuhusiana na ongezeko la uhalifu hayana mashiko. Wanasema uamuziwake huo ni mbinu ya kujijenga kisiasa kwa ajili ya uchaguzi wa Novemba, hasa baada ya kadhia ya virusi vya korona kuathiri pakubwa mtazamo wa wapigakura kumhusu rais huyo

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages