Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul
Makonda (watatu
kushoto), akipokea mfano wa ufunguo wa kari kuashiria makabidhiano rasmi wa
gari gari Moja kati ya mbili walizoahidi kumpatia kama sehemu ya Mchango
katika mapambano dhidi ya Corona katika Mkoa huo. Wengine pichani kutoka
kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha
Rasilimali watu wa kampuni ya utengenezaji wa magari aina ya TATA, Thomas Macha
na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (RMO) ,Dkt. Rashid Mfaume
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda (kushoto)
akipata maelezo kutoka ka Mkurugenzi wa Kitengo cha Biashara wa Kampuni ya TATA
Motors, Rajiv Bhushan wakati wa hafla ya kumkabidhi Mkuu wa Mkoa gari Moja kati
ya mbili walizoahidi kumpatia kama sehemu ya Mchango katika mapambano dhidi ya
Corona katika Mkoa huo. Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (RMO)
,Dkt. Rashid Mfaume pamoja TATA na Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali watu wa
kampuni ya, Thomas Macha. Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika leo katika
ofisi za Tata zilizobo vingunguti.
Mkuu wa
Kitengo cha Rasilimali watu wa kampuni ya utengenezaji wa magari aina ya TATA,
Thomas Macha, akizungumza wakati wa hiyo.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Biashara wa Kampuni ya TATA Motors, Rajiv
Bhushan akizungumza katika warsha hiyo. Picha zote na Brian Peter
Kampuni ya Kimataifa ya Magari ya TATA Africa Holding Ltd leo
imemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda Gari Moja kati ya
mbili walizoahidi kumpatia kama sehemu ya Mchango katika mapambano dhidi ya
Corona katika Mkoa huo.
Gari hiyo aina ya XENON X2 Double Cabin RC Makonda ameelekeza
itumike kuwasafirisha Watumishi wa Afya wanaofanya kazi ya Mapambano dhidi ya
Corona.
Aidha RC Makonda ameishukuru kampuni hiyo kwa mchango walioutoa
na kusema Gari hiyo itaenda kutatua changamoto za usafiri zilizokuwa zikiwakabili
watumishi wa Sekta ya Afyahuku akieleza kuwa hali ya Maambukizi ya Corona
katika Mkoa huo imepungua na Wagonjwa wengi wanazidi kupona.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya TATA Motors, Bwana Rajiv
Bhushan amesema kwa siku ya leo wamekabidhi Gari moja ambapo Gari ya pili
wataikabidhi muda wowote kuanzia sasa.
Aidha Bw.Rajiv amesema Kampuni hiyo imeona ni vyema ikawa sehemu
ya mchango kwa jamii katika mapambano dhidi ya Corona kwa kuhakikisha watoa
huduma wa Afya wanakuwa na usafiri wa uhakika.
No comments:
Post a Comment