A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, April 16, 2020

Runinga ya Kenya yajuta kumuita rais Magufuli 'Mkaidi'

Runinga yenye watazamaji wengi nchini Kenya imesema katika taarifa iliotangazwa katika chumba hicho cha habari kwamba inajuta kumuita rais Magufuli 'mkaidi' , katika ripoti yake iliozungumzia kuhusu sera zake katika kukabiliana na mlipuko wa virusi vya corona.

Tanzania haijaweka masharti makali kuhusu mikutano ya watu kama ilivyofanywa na mataifa mengine duniani.

Katika ripoti hiyo ya runinga ya Citizen iliopeperushwa hewani tarehe 22 mwezi Machi , bwana Magufuli alinukuliwa akisema kwamba mlipuko wa virusi vya Covid-19 haufai kutumiwa kama sababu ya kuathiri uchumi wa Tanzania.

Runinga hiyo inayopeperusha matangazo yake katika eneo la Afrika Mashariki , ilisema katika ripoti hiyo kwamba haikuwa na madhumuni ya kuwapotosha raia wa Tanzania.

Taarifa hiyo ilisema :
Tunanukuu: Tarehe 22 Machi , tuliripoti kuhusu mipango iliowekwa na serikali ya Tanzania kukabiliana na janga la virusi vya corona. Katika ripoti hiyo tulimuita rais Magufuli 'mkaidi'.

Tunanukuu ujumbe: Katika mahojiano na runinga ya Citizen , balozi wa Tanzania nchini Kenya alisema kwamba Magufuli anaunga mkono juhudi za kieneo na kimataifa kukabiliana na mlipuko wa virusi vya corona .

Tunanukuu ujumbe: Utumizi wa neno 'mkaidi' dhidi ya rais Magufuli hauna msingi .

Idadi ya wagonjwa Tanzania yafikia 88 baada ya wengine 29 kuthibitishwa
Serikali ya Tanzania ilithibitisha wagonjwa 29 wapya wa virusi vya corona siku ya Jumatano .

Kulingana na taarifa ya wizara ya Afya nchini humo wagonjwa 26 kati yao wapo katika mji wa Dar es Salaam huko wawili wakipatikana mjini Mwanza na mmoja akiwa katika eneo la Kilimanjaro.

Waziri wa Afya Ummi Mwalimu alisema kwamba ufuatilianaji wa watu waliokaribiana na wagonjwa hao unaendelea.

Hatahivyo waziri huyo alitangaza habari njema akisema kwamba hadi kufikia Jumatano takriban watu 11 wamepona virusi hivyo lakini akaongezea kwamba watu wanne walifariki.

Ongezeko hilo la wagonjwa linajumlisha wagonjwa wapya sita waliotangazwa na waziri wa Afya wa kisiwa cha Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages