A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, March 13, 2020

VODACOM KUSAIDIA SEKTA YA ELIMU KUPITIA TEHAMA

Mkurugenzi wa Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania PLC, Rosalynn Mworia (katikati) akielezea namna Vodacom walivyojidhatiti kuhakikisha TEHAMA inasaidia sekta ya elimu kupitia mtandao wa Vodacom kwenye kongamano la wadau wa Elimu lililoenda sambamba na maadhimisho ya Wiki ya Ubunifu nchini. Kulia ni Mwalimu wa Tehama kutoka shule ya msingi Mafinga mkoani Iringa, Apia Lugenge na Mshauri toka UNESCO, Basilina Levira.
Mwanafunzi wa shule ya Sekondari Jangwani, Charity Luckson akichangia mada kwenye kongamano la Elimu lililofanyika leo jijini Dar Es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Uzalishaji kwa Wateja Wakubwa Ali Z. Ali wa Vodacom Tanzania PLC akielezea namna Shule ndani ya boksi ‘School in a box’ inavyoweza kuhifadhi nishati ya umeme na kutumika kufundishia katika maeneo ambayo yana upungufu wa Walimu na vifaa vya kufundishia.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages