Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya magari ya Scania Tanzania Ltd,
Lars Eklund, akizungumza wakakati wa kampuni hiyo kutangaza kuleta mabasi
yatumiayo gesi asilia ambayo ni bora kwa soko la Tanzania hasa kwa usafiri wa
umma (Bus RapidTransit) hafla hiyo ilifanyika katika ofisi kuu ya Scania
iliyoko vingunguti jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya magari ya Scania Tanzania Ltd,
Lars Eklund, akizungumza wakakati wa kampuni hiyo kutangaza kuleta mabasi
yatumiayo gesi asilia ambayo ni bora kwa soko la Tanzania hasa kwa usafiri wa
umma (Bus RapidTransit) hafla hiyo imefanyika leo katika ofisi kuu ya Scsnia
iliyoko vingunguti jijini Dar es Salaam. Mwengine pichani ni Meneja Masoko wa
Scania, Eliavera Timoth. Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi kuu ya Scania
iliyoko vingunguti jijini Dar es Salaam.
Meneja Masoko wa Kampuni ya Scania Tanzania Ltd, Eliavera
Timoth (kulia), akizungumza wakakati wa kampuni hiyo kutangaza kuleta
mabasi yatumiayo gesi asilia ambayo ni bora kwa soko la Tanzania hasa kwa
usafiri wa umma (Bus RapidTransit) hafla hiyo imefanyika leo katika ofisi kuu
ya Scsnia iliyoko vingunguti jijini Dar es Salaam kulia kwake ni Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni ya magari ya Scania Tanzania Ltd, Lars Eklund hafla hiyo
ilifanyika katika ofisi kuu ya Scania iliyoko vingunguti jijini Dar es
Salaam.
Na Mwandishi wetu;
Kampuni ya magari ya Scania Tanzania Ltd yatangaza kuleta mabasi
yatumiayo gesi asilia ambayo ni bora kwa soko la Tanzania hasa kwa usafiri wa
umma (Bus Rapid Transit). Bidhaa hii ni sehemu ya juhudi ya kampuni kuhakikisha
inaongoza katika kuboresha sekta ya usafirishaji nchini. Kampuni ya Scania
inaamini kuwa ni wakati sahihi kwa Tanzania kuingiza katika mfumo huu na
mingine kwa ajili ya kuboresha maisha ya watu kimazingira na kiuchumi.
Tanzania ina akiba kubwa ya gesi asilia na inahitaji maelfu ya mabasi
ya jiji kwa mfumo wa BRT ambayo kampuni ya Scania inaweza kuleta. Kampuni ya
Scania imekuwa imefanikiwa kuleta magari ya mfumo wa gesi kwa muda mrefu sehemu
mbalimbali duniani kama Amerika Kusini, Ulaya na Australia.
Moja ya faida ya mabasi yanayoendeshwa na mfumo wa gesi asilia
(Compressed Natural Gas) ni kwamba mfumo wake wa injini utasaidia kupunguza
hewa chafu (Carbon dioxide) kwa asilimia 20 ambapo CO2 inatajwa kuwa ndio
chanzo cha joto kali duniani, itapunguza gharama za uendeshaji, gharama kwa abairia
na itasaidia serikali kuongeza mapato kupitia uuzaji wa gesi asilia.
Akizungumza na wanahabari katika ofisi kuu iliyoko Vingunguti kando na
barabara ya Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Scania
Tanzania, Lars Eklund amesema Tanzania inaelekea kuwa nchi ya viwanda, hivyo
ufanisi unahitajika na kwamba mazingira yasisahaulike.
“Tunaamini ya kwamba Tanzania inahitaji kuwa na teknolojia mpya ili
iendane na kasi ya nchi zilizoendelea. Tanzania ni tajiri sana kwa gesi asilia
na ni muhimu kutumia nishati hii ya ndani kwa faida ya nchi, nchi itapata faida
sana kwani itapunguza kiasi cha mafuta yanayoagizwa nje” na badala yake inaweza
kuuza gesi ya ndani kwa waendeshaji wa ndani. Hakuna njia bora na ni ghari sana
kujaribu kubadili injini ya dizel kuwa injini ya gesi. Alisema Bwana Lars
Eklund.
Kumekuwa na taaria kupitia vyombo vya habari kutaka kubadili mfumo wa
sasa wa magari ya BRT kutoka injini ya dizel kwenda injini ya gesi, suala hili
halina tija kiufundi na kiuchumi kwa sababu injini ya dizeli imeundwa kufanya
kazi katika mzunguko wa dizeli wakati injini za gesi na petrol zinaendeshwa
kulingana na kanuni ya Otto na ujazo wa kuziba cheche. Kwa hiyo ni muhimu sana
kuwepo kwa mipango bora ya upanuzi wa miundo mbinu ya gesi asili ambapo
itasaida wauzaji na waendeshaji kuthubutu kuwekeza katika bidhaa sahihi za gesi
asilia zitakazotumiwa barabarani haraka iwezekanavyo. Alisema Bwana Lars
Eklund.
Kama sehemu ya kukuza huduma zake nchini, kampuni ya Scania Tanzania
inatafuta kushirikiana na taasisi mbalimbali za elimu kufadhili wanafunzi
wanaochukua elimu kuhusu matumizi ya gesi asilia (Compressed Natural Gas). Hii
itasaidia kuongezeka kwa idadi ya mafundi na wataalamu katika uwanja huo hivyo
kuongezeka kwa msaada kwa watumiaji wa mabasi yenye mfumo wa gesi nchini.
Mpango huu sio tu sehemu ya kujitolea kuboresha huduma lakini pia ni njia ya
kurudisha fadhila kwa jamii zetu zinazotuzunguka. Alisema Bwana Eliavera
Timoth, Meneja Masoko Scania Tanzania.
KUHUSU SCANIA TANZANIA LIMITED
Kampuni ya Scania Tanzania inafanya kazi kama kampuni ndogo ya Scana CV
AB yenye makao makuu yake nchini Sweden. Kampuni ya Scania Tanzania
inajihusisha na uingizaji na usambazaji wa bidhaa za Scania nchini. Kampuni hii
ina ofisi sehemu mbalimbali nchini ambapo makao makuu yake ni Dar es Salaam,
huku ofisi nyingine ni Mwanza, Arusha na Mbeya.
No comments:
Post a Comment