Dar es Salaam, 16/10/2019: Benki ya NMB imezindua malipo ya kimtandao kwa huduma za bodaboda.
Mfumo huo wa malipo ni wa aina yake na wa kwanza nchini unaowawezesha abiria na wateja wa bodaboda kulipa nauli zao kwa kutumia simu zao za mkononi na fedha hizo kwenda moja kwa moja kwenye akaunti ya NMB ya dereva husika.
Huduma hii iliyozinduliwa ni mwendelezo wa juhudi za kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanatumia huduma za benki sambamba na kuhamasisha utunzaji fedha kwa njia salama na za uhakika.
Akizungumza kwenye uzinduzi wa huduma hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama alisema huduma hii inaweka msingi wa kurasimisha sekta ndogo ya usafiri wa bodaboda.
"Mnachokifanya leo kina baraka zote za Serikali. Hiki kitawasaidia vijana kuongeza umakini kwenye shughuli zao na kuchangia uchumi wa Taifa," amesema Mhagama.
Mfumo huo wa malipo ni wa aina yake na wa kwanza nchini unaowawezesha abiria na wateja wa bodaboda kulipa nauli zao kwa kutumia simu zao za mkononi na fedha hizo kwenda moja kwa moja kwenye akaunti ya NMB ya dereva husika.
Huduma hii iliyozinduliwa ni mwendelezo wa juhudi za kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanatumia huduma za benki sambamba na kuhamasisha utunzaji fedha kwa njia salama na za uhakika.
Akizungumza kwenye uzinduzi wa huduma hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama alisema huduma hii inaweka msingi wa kurasimisha sekta ndogo ya usafiri wa bodaboda.
"Mnachokifanya leo kina baraka zote za Serikali. Hiki kitawasaidia vijana kuongeza umakini kwenye shughuli zao na kuchangia uchumi wa Taifa," amesema Mhagama.
No comments:
Post a Comment