A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, September 13, 2019

MHESHIMIWA WAZIRI LUKUVI AZINDUA ULIPAJI KODI YA ARDHI KWA AIRTEL MONEY

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza wakati wa kuzindua huduma ya ulipaji kodi ya pango la ardhi kupitia Airtel Money katika ofisi za Wizara eneo la Mtumba jijini Dodoma. Wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Beatrice Singano na kulia ni Meneja wa Huduma kwa Wateja Airtel mkoa wa Dodoma Delphina Msangi.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akiongea na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Beatrice Singano wakati wa kuzindua huduma ya ulipaji kodi ya pango la ardhi kupitia Airtel Money katika ofisi za Wizara eneo la Mtumba jijini Dodoma.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amezindua huduma ya ulipaji kodi ya pango la ardhi kwa kutumia mtandao wa simu ya mkononi kupitia Airtel Money.

Uzinduzi wa ulipaji kodi ya pango la ardhi kwa njia ya Airtel Money unarahisisha huduma hiyo ambapo wamiliki wa ardhi wataweza kufanya malipo kupitia mtandao huo wa simu bila kwenda ofisi za Ardhi.

Akizungumza jijini Dodoma jana tarehe 9 Septemba 2019 wakati wa kuzindua huduma hiyo, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alisema ubunifu wa serikali kufanya malipo ya Ankara za serikali kwa kutumia mfumo wa GePG umerahisisha malipo ya tozo mbalimbali za serikali ikiwemo kodi ya pango la ardhi.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages