WATU wanne wamefariki dunia katika ajali iliyohusisha basi la abiria mali ya Kampuni ya Safari Njema lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Dodomana lori  maeneo ya Nanenane mjini Morogoro usiku wa kuamkia leo.

Jeshi la Polisi limethibitisha kwamba:  “Ni kweli usiku wa kuamkia leo Ijumaa Agosti 16, 2019, majira ya saa 7:30, kumetokea ajali eneo la Nanenane, basi mali ya Safari Njema likitokea Dar kwenda Dodoma limegongana kwa ubavu na lori mali ya Tumbaku Alliance, watu wanne wamefariki akiwemo dereva wa lori.”