A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, April 25, 2019

WATEJA WA TIGO WILAYANI KILOLO, MKOANI IRINGA WAPATA HUDUMA YA KASI ZAIDI YA 3G

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Kililo Mkoani Iringa Philemon Namwenga (wa tatu kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mnara mpya wenye uwezo wa 3G katika kijiji cha Idete, Wilaya Kilolo, mkoani Iringa mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Meneja wa Tigo kanda ya Kusini Abbas Abdurahamani na wa kwanza kulia ni diwani wa viti maalum kata ya Idete Elina Kivegele na anayemfuatia ni Meneja Mauzo wa Tigo Iringa, Samwel Chanai.
Meneja wa Tigo kanda ya Kusini Abbas Abdurahamani (kushoto) akibadilishana mawazo na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Kililo Mkoani Iringa Philemon Namwenga (wa pili kulia) muda mfupi baada ya uzinduzi wa mnara mpya wenye uwezo wa 3G katika kijiji cha Idete wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa. Wa kwanza kushoto ni Meneja Mauzo wa Tigo Iringa, Samwel Chanai diwani wa viti maalum kata ya Idete Elina Kivegelea.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa Philemon Namwenga pamoja na Meneja wa Tigo kanda ya Kusini Abbas Abdurahamani, wakisalimiana na wananchi wa kijiji cha Idete Wilayani Kilolo mkoani Iringa muda mfupi baada ya uzinduzi wa manra mpya wenye uwezo wa 3G kijijini hapo.
Meneja wa Tigo kanda ya Kusini Abbas Abdurahamani (wa pili kushoto) akimuonyesha Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa Philemon Namwenga baadhi ya smart phone za gharama nafuu zinazouzwa na kampuni ya Tigo muda mfupi baada ya uzinduzi wa mara mpya wenye uwezo wa 3G katika kijiji cha Idete wailayani Kilolo. Wa kwanza kulia ni Meneja Mauzo wa Tigo Iringa, Samwel Chanai.
Kampuni ya mawasiliano ya simu, Tigo, imezindua mnara wa 3G katika kata ya Kidete, mkoani Iringa kama moja ya jitihada zake za kufikisha huduma bora za kupiga na kupokea simu, intaneti na kutuma na kupokea pesa kwa wateja wake.

Akizungumza katika uzinduzi huo katika kata ya Idete, Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Kilolo, Aloyce Kwezi, aliwakaribisha na kuwashukuru Tigo kwa kuongeza ufanisi wa mnara huo kutoka teknolojia ya 2G hadi 3G.


Serikali ya Tanzania imefanya suala la viwanda kuwa agenda yake kuu. Na sisi kama serikali tunatambua umuhimu wa mawasiliano katika kufanikisha hii dira. Tunapenda kuwashukuru sana kwa kuifikiria Kilolo na wananchi wake, maana sekta hii ya mawasiliano ni chachu kubwa sana katika ukuaji na ubunifu wa viwanda mbalimbali,” alisema Kwezi.
Kwa upande wake, Meneja wa Tigo Kanda ya Kusini, Abbas Abdurahamani, alisema kwamba kipaumbele ya Tigo ni kuhakikisha kwamba wateja wake wanapata huduma za kisasa za kiteknolojia za simu kama ya 3G.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages