A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, May 14, 2018

WAITARA MBUZI CUP YATIMUA VUMBI KIVULE

Mchezaji wa timu ya Magole Fc, Abdallah Ally (kushoto) akijaribu kumtoka mchezaji wa timu ya Stonefire Fc, Abdallah Sultan katika mchezo wa fainali ya Ligi ya Waitara Mbuzi Cup iliyochezwa katika Uwanja wa Magole kwa Mama Anna Mkapa jijini Dar es Salaam. Stonefire Fc ilishinda Magole Fc kwenye matuta kwa bao 4-2.
Mchezaji wa Timu ya Stonefire Fc, Sudy Manyama (kulia) akichuana Vikali na  Mchezaji wa timu ya Magole Fc,Msafiri Oscar katika mchezo wa fainali ya Ligi ya Waitara Mbuzi Cup iliyochezwa katika Uwanja wa Magole kwa Mama Anna Mkapa jijini Dar es Salaam.
Diwani wa Kata ya Kivule,Wilson Molel (kushoto) akizungumza jambo na Vijana wa kata hiyo jijini Dar es Salaam katika mchezo wa fainali ya ligi ya Waitara Mbuzi Cup iliyochezwa katika Uwanja wa Magole kwa Mama Anna Mkapa jijini Dar es Salaam leo.Ligi hiyo inayodhaminiwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga,M wita Waitara.Wapili kushoto ni Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Singo Benson,Katibu Mwenezi wa Chadema kata ya Kivule,Bihimba Nassoro na Mwenyekiti Chadema kata ya Kivule, Kisiri Anthony.
Mwakilishi wa Mbunge wa Jimbo la Ukonga pia ni Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Singo Benson (wapili kushoto) akizungumza na wakazi wa kata ya Kivule jijini Dar es Salaam leo katika hafla ya kukabidhi mbuzi kwa mshindi wa kwanza wa ligi ya Waitara Mbuzi Cup iliyofanyika katika uwanja wa Magole kwa Mama Anna Mkapa jijini Dar es Salaam.
Diwani wa Kata ya Kivule,Wilson Molel (wapili kushoto), pamoja na Mwakilishi wa Mbunge wa Jimbo la Ukonga pia ni Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Singo Benson  wakikabidhi mbuzi kwa Kapteni wa timu ya Stonefire Fc baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika fainali ya ligi ya Waitara Mbuzi Cup kwa kuipiga bao 4-2 Timu ya Magole Fc katika Uwanja wa Magole kwa Mama Anna Mkapa jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Mbunge wa Jimbo la Ukonga pia ni Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Singo Benson (kulia) akikabidhi mpira kwa Kapteni wa Timu ya Magole Fc, Isack Mairi baada ya kuibuka mshindi wa pili katika fainali fainali ya ligi ya Waitara Mbuzi Cup iliyodhaminiwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga Mwita Waitara.Katikati ni Diwani wa Kata ya Kivule,Wilson Molel.
      Mwenyekiti Chadema kata ya Kivule,Kisiri Anthony akizungumza katika hafla hiyo.
Katibu Mwenezi wa Chadema kata ya Kivule,Bihimba Nassoro akitoa shukrani za dhati kwa timu zilizoshiriki katika ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages