A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, May 23, 2018

Uhalifu wapungua Upanga Mashariki




Na Heri Shaaban




SERIKALI ya Mtaa ya Upanga Mashariki imesema vitendo vya uhalifu katika mtaa wao kwa sasa vimepungua baada kuanzishwa Ulinzi Shirikishi wa madereva wa bodadoda wa mtaa huo.

Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana, na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa huo Rukiya Ritani, wakati wa kuzungumza na waandishi wa habari kuelezea mafanikio ya mtaa wake.

"Tumeanzisha Polisi jamii katika mtaa wetu  jeshi letu la madereva wa bodaboda  wanafanya kazi zao kwa umakini kwa sasa vitendo vya uhalifu amna tukio la uhalifu likitokea wanawakamata watuhumiwa  alafu wanapelekwa polisi"alisema Rukiya .

Rukiya alisema wananchi wake wa mtaa huo kwa ushirikiano wa Wajumbe wake wa serikali ya mtaa wanashirikiana na Polisi Jamii katika kulinda rahia na mali zao.

Alisema kwa sasa mafanikio makubwa ambayo yamepatikana wananchi wanapita bila kupolwa barabarani mali zao.

Alisema mtaa huo una wakazi  4800  changamoto iliyokuwepo  walipaji ada wachache amewataka wananchi kulipa ada ya ulinzi kwa wakati ili iweze kuwasaidia polisi jamii wao ambao wanafanya  kazi hiyo ya kujitolea.

 Akielezea changamoto nyingine wanachi wa mtaa huo wamekuwa wavivu katika  kushiriki vikao vya maendeleo   jambo linapotokea katika mtaa mengi wanaoitwa.


Kwa upande wake kiongozi  wa Ulinzi shirikishi Upanga Mashariki, Seleman Abdalah alisema  asilimia 85 uhalifu  umepungua.

Abdallah alisema kwa sasa Upanga Mashariki mpya jeshi lake  limejipanga vizuri wanashirikiana na Polisi wakati wa matukio ya uhalifu yakitokea.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages