A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, May 14, 2018

Shilole afunguka kupewa Tuzo na Aunty Ezekiel

 Muigizaji Aunty Ezekiel siku ya May 13, 2018 alimpatia tuzo ya heshima muigizaji na muimbaji wa bongofleva Shilole kutokana na juhudi zake kama Mama na jinsi anavyopambana kwenye malezi ya wanae huku akiongeza juhudi zake kwenye kujishughulisha zaidi kuhakikisha wanae wanasoma shule nzuri.

Tuzo hiyo aliyopewa Shilole ilitolewa siku ya Mama duniani ambapo ndiyo siku ambayo Aunty Ezekiel alizindua short Film yake ya Mama ikiwa ni ujumbe kuhusu kwa wa mama wote Duniani na namna wanavyopambana kulea watoto wao katika mazingira magumu.

Wakati wa ukabidhiwaji wa Tuzo hiyo Shilole hakuwepo hivyo Snura akamuwakilisha na ndipo leo kupitia Instagram page ya Shilole ameamua kuandika haya...”Naamini wapo wengi mno waliostahiri, lakini siwezi kuwa na maneno ya kutosha kukushukuru kwa heshima kubwa uliyonipa Mama Cookie.”

“Asante kwa zawadi nzuri, heshima na Tuzo ya mama mpambanaji bora kwa bongo flavour na movie, ktk uzinduzi wako wa filamu ya Mama. Lkn pia hongera kwa kazi nzur na product ya body spray uliyoizindua wewe ni Mwanamke Shupavu.”

“Mama yangu Aliniacha nikiwa mdogo sn nikaelewa ilivyo vigumu kuishi bila Mama. Ndio maana Pamoja na yooote Nitapambana kwaajili ya wanangu. Ukiwagusa wanangu, Umenigusa mimi. Ndio watu pekee naoweza kusema Nipo tayar kufa kwaajili yao.” – Shilole


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages