Naibu mkufunzi wa klabu ya Manchester City Mikel Arteta ni miongoni mwa wakufunzi wanaopigiwa upatu kumrithi mkufunzi wa Arsenal anayeondoka Arsene Wenger.
Raia huyo wa UHispania ambaye aliichezea The Gunners mara 150 alianza kuwa naibu wa kocha katika klabu ya City 2016.
Hakuna makubaliano yalioafikiwa kufikia sasa kuhusu mkufunzi aliyechaguliwa na kwamba klabu hiyo haijakuwa tayari kuajiri kocha mpya.
Hatahivyo klabu hiyo ina matumaini kwamba itamtaja mrithi wa Wenger kabla ya kombe la dunia linaloanza Juni 14.
Uamuzi utakapoafikiwa na afisa mkuu mtendaji Ivan Gazidis , mkuu wa uhusiano wa soka Raul Sanllehi na mkuu wa usajili Sven Mislintat , watatu hao watawasilisha mapendekezo yao kwa bodi ya Arsenal ili wakurugenzi kuidhinisha.
Wenger ataisimamia Arsenal kwa mara ya mwisho siku ya Jumapili dhidi ya Huddersfield baada ya miaka 22 katika uongozi wake.
Kocha wa zamani wa Barcelona Luis Enrique pia amehusishwa na kazi hiyo pamoja na mkufunzi wa Juventus Massimiliano Allegri.
Kulingana na mwandishi wa habari za michez wa BBC David Ornstein Allegri ndiye anayepigiw upatu na wchanganuzi lakini Arteta ameorodheshwa na ijapokuwa Arsenal inasema kuwa wawili hao ndio huenda wakachukua wadhfa huo sio wakufunzi pekee walioorodheshwa.
Post Top Ad
Your Ad Spot
Sunday, May 13, 2018
Mikel Arteta aweza kumrithi Arsene Wenger Arsenal
Tags
MICHEZO#
Share This
About kilole mzee
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment