A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, May 14, 2018

MBOWE ATILIA MKAZO KAULI MBIU YA ‘‘MICHEZO NI AJIRA’’ KIVULE

Mchezaji wa timu ya Songas Fc, Frank Skanyika (kushoto) akichuana vikali na Mchezaji wa Timu ya Wafanyabiashara wa Kivule Fc, Salum Machaku katika mchezo wa fainali ya ligi ya Waitara Mbuzi Cup iliyochezwa katika uwanja wa Kivule jijini Dar es Salaam. Timu ya Wafanyabiashara wa Kivule Fc iliwapiga kwa matuta timu ya Songas Fc bao 3-2.
Mchezaji wa timu ya Songas Fc,Jovin Joseph (kulia) akijaribu kumtoka mchezaji wa timu ya Timu ya Wafanyabiashara wa Kivule Fc, Mkwaya Hula katika mchezo wa fainali ya ligi ya Waitara Mbuzi Cup iliyochezwa katika uwanja wa Kivule jijini Dar es Salaam.
Diwani wa kata ya Kivule,Wilson Molel akizungumza na wakazi wa Kivule jijini Dar es Salaam katika fainali ya ligi ya Waitara Mbuzi Cup kati ya Timu ya Wafanyabiashara wa Kivule Fc na Songas Fc iliyochezwa katika uwanja wa Kivule.Ligi hiyo imedhaminiwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mhe.Freeman Mbowe  (wapili kulia) akizungumza na Wakazi pamoja na wafanyabiashara wa Kivule jijini Dar es Salaam leo baada ya kuwasili katika kata hiyo kwa ajili ya kushuhudia pamoja na kukabidhi zawadi ya Mbuzi kwa mshindi wa kwanza wa Ligi ya Waitara Mbuzi Cup iliyochezwa katika uwanja wa Kivule.Huu ni mwendelezo wa Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara kutimiza ahadi alizoahidi kwa vijana katika kuisapoti sekta ya michezo jimboni.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe (wapili kushoto) akikabidhi mbuzi kwa Kapteni wa timu ya Wafanyabiashara wa Kivule jijini Dar es Salaam leo baada ya kuibuka kidedea kuipiga timu ya Songas Fc kwa matuta bao 3-2 katika fainali ya ligi ya Waitara Mbuzi Cup iliyochezwa katika uwanja wa Kivule. Wapili kulia ni Diwani wa kata ya Kivule, Wilson Molel.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),Freeman Mbowe (katikati) akikabidhi mpira kwa Kapteni wa timu ya Songas Fc baada ya kushika nafasi ya pili katika fainali ya ligi ya Waitara Mbuzi Cup iliyochezwa katika uwanja wa Kivule jijini Dar es Salaam.
Katibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kata ya Kivule, Bihimba Nassoro (kulia) akizungumza na wachezaji wa mpira wa miguu pamoja na Viongozi wa Chadema baada ya fainali ya ligi ya Waitara Mbuzi Cup kumalizika kati ya Wafanyabiashara wa Kivule Fc na Songas Fc ilyochezwa katika Uwanja wa Kivule jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Mwenyekiti wa Chadema kata ya Kivule, Kisiri Anthony.
Wachezaji pamoja na mashabiki wa Timu ya Wafanyabiashara wa Kivule Fc wakishangilia baada ya kukabidhiwa mbuzi na Viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo kwa niaba ya Mbunge wa Jimbo la Ukonga,Mwita Waitara jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages