A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, May 28, 2018

KAMATI YA MAAFA MKOA WA DAR ES SALAAM YAZIFIKIA KAYA 600 ZILIZOKUMBWA NA MAFURIKO


Mkurugenzi wa Taasisi ya Abdulah Aid, Arif Abdurrahimani, akizungumza na waandishi wa habari habari.

Kamati ya  ya kutoa misaada ya kibinadamu iliyo undwa  na  Mkuu wa mkoa wa Dar es salaa mhe . Paul Makonda  kwaajili ya kutoa  msaada kwa waathirika wa mafuriko mkoa wa Dar es salaam , imesema imekamilisha zoezi hilo kwa kuwafikia walengwa wote ambao walipata atha hiyo.

Akizungumza na wa waandishi wa habari  mwenyekiti wa  kamati hiyo Ubaya Chuma  amesema  waathika wote walikuwa wametambuliwa wamefikiwa na misaada mbambali ya kibinaadamu ikiwemo kupatiwa Magodoro, vyakula  mbalimbali kama Maharage , Mchele,Unga wa ngano na wa mahindi  Sukari na mafuta ya kupikia na mahitaji mengine mengi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Abdulah Aid, Arif Y. Abdurrahimani ameseama katika kuwapatia watu hao misaada Taasisi mbalimbali zimeshiriki ikiwemo, Taasisi ya  Miraji Islamic Center ya Zanzibar , Taasisi ya Abdulla AID  na Taasisi yake ,amesema wamefurahishwa  na huduma hiyo  na wameweza kuzifikia  kaya 600 kutoka maeneo mbalimbali katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Akisoma taarifa ya kamati hiyo George Shinga Mtambalike amesema  Jumla  ya vitu vilivyotolewa na Taasisi hizo ni pamoja na  kilo 2400 za mchele,kilo 360 za Sukari, Mafuta ya kupikia Lita 600,kilo 600 za Maharagwe na kilio600 za Unga wa mahindi.

Aidha amesema misaada mingine iliyo tolewa ni pamaoja  na Magodoro 490, mito ya kulalia 490 ,Mashuka 490 pamoja na Net za Mbu.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages