A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, March 8, 2018

Mvua yaleta athari kubwa kwa Jeshi la Polisi



Mvua zilizoambatana na upepo mkali zilizonyesha usiku wa jana zimeacha athari kubwa kwa Jeshi la Polisi kwa kuharibikiwa na jengo lao la ofisi pamoja na kujeruhiwa askari mmoja.

Akizungumza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni,  ACP Muliro Jumanne Muliro amekiri kutokea kwa tukio hilo na kusema ofisi ndogo iliyopo ndani ya jengo la serikali ya Mtaa wa Goba limeharibika kufuatia kuangukiwa na nguzo ya mnara wa simu kuangukia.

"Askari mmoja amejeruhiwa katika ajali hiyo ila alifanikiwa kukimbizwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu", amesema Kamanda Muliro.

Mbali na tukio hilo, mvua zilizonyesha usiku wa jana (Machi 07, 2018) zimeweza kuwaathiri pia baadhi ya jamii kwa kuezua paa za nyumba zao na kusababisha kukosa makazi.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages