A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, February 1, 2018

RC MAKONDA AKOSHWA NA KASI YA UJENZI WA OFISI ZA MAKAO MAKUU YA BAKWATA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Ofisi za Makao Makuu ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania BAKWATA ambapo amefurahishwa na kasi ya ujenzi huo.

Ujenzi wa jengo hilo la kisasa ni jitiada za RC Makonda kuthamini na !kuwapa heshima Viongozi wa Dini kwa kuhakikisha wanafanyakazi katika mazingira mazuri na yenye hadhi kutokana na thamani na mchango wao mkubwa katika jamii. 

Jengo hilo la kisasa lenye Gorofa Nne pamoja na Ground floor lina Ofisi ya Mufti wa Tanzania, Ofisi ya katibu, VIP room, kumbi za mikutano, Ofisi za wafanyakazi, ofisi za mshauri,Jiko,Vyoo, sehemu ya Kufanya Dua pamoja sehemu ya Mapokezi. 

RC Makonda amesema kazi wanayofanya Viongozi wa Dini ni kubwa hivyo tunapaswa kuthamini kwa kuwaweka mazingira mazuri ya kufanya kazi. 

Aidha RC Makonda amesema shauku yake ni kuona hadi mwezi wa Ramadhani jengo linakuwa limekamilika na kuanza kutumika. 

Aidha RC Makonda amewaomba Viongozi wa Dini kuendelea kuliombea Amani Taifa na viongozi wake.

Kwa upande wake Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuber amemshukuru RC Makonda kwa kuwajengea jengo hilo na kusema katika Miaka 50 BAKWATA haijawahi kuwa na jengo zuri na lakisasa Kama hilo hivyo RC Makonda anaweka historia ya kwanza.

Mufti amesema jengo lililokuwepo lilikuwa likiwafanya kuona hata haibu hata kupokea ugeni wa viongozi wa kislamu ulimwenguni.


Katika ziara hiyo Viongizi wa Dini kwa pamoja wamemuombea Dua RC Makonda pamoja na Rais Dr. John Magufuli kwa kuwezesha kujengwa kwa msikiti wa Mfalme wa Morocco wenye uwezo wa kuchukuwa watu 8,000 ampapo ujenzi unaendelea. 

MATUKIO KATIKA PICHA RC MAKONDA AKIKAGUA UJENZI HUO

  Makonda akiwasili katika ofisi zinazojengwa


 Rc Makonda akisalimiana na Shekh Mkuu wa Tanzania



 Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuber akizungumza jambo katika hafla hiyo.

 Rc Makonda akipata maelezo kutoka kwa mafundi wa ujenzi huo
Ukafika wakati wa dua kuombea ujenzi huo usiwe na vikwazo

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages