A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, February 21, 2018

RC MAKONDA AFANYA ZIARA KATIKA SHULE YA MBANDE NA MAJIMATITU TEMEKE.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akizungumza na wananchi walimu pamoja na wanafunzi katika shule ya msingi Mbande iliyopo katika Halmashauri ya temeke nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam alipofanya ziara  ya kukagua mpango mkakati wa halmashahuri hiyo wa kutatua changamoto zilizopo katika shule za Msingi Mbande na maji matitu zenye wanafunzi wengi waliojitokeza kujiandikiasha na darasa la kwanza kwa mwaka 2018. (kushoto) ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva  na kulia ni Diwani wa kata hiyo Hemmed Karata, pamoja na viongozi wengine wa kata hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva (kulia) akizungumza na wanainchi walimu pamoja na wanafunzi katika shule ya msingi Mbande iliyopo katika Halmashauri ya temeke nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam kwenye ziara ya Mkuu wa Mkoa alipofanya ziara  ya kukagua mpango mkakati wa halmashahuri hiyo wa kutatua changamoto zilizopo katika shule za Msingi Mbande na maji matitu zenye wanafunzi wengi waliojitokeza kujiandikiasha na darasa la kwanza kwa mwaka 2018.wa tatu kushoto ni Mkuu wa Mkoa Paul Makonda kulia kwa Makonda ni Diwani wa kata ya Kirungule Saidi Fella na Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo.
Kaimu Afisa Elimu Msingi Sylvia Mutasingwa, akitoa taarifa ya uandikishwaji wawanafunzi  wa darasa la kwanza mwaka 2018kwakuwa  imeonesha kuwa wilaya hiyo inaongoza kwakuwa na wanafuzi wengi katika shule ya msingi Mbande iliyopo katika Halmashauri ya temeke nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam kwenye ziara ya Mkuu wa Mkoa alipofanya ziara  ya kukagua mpango mkakati wa halmashahuri hiyo wa kutatua changamoto zilizopo katika shule za Msingi Mbande na maji matitu zenye wanafunzi wengi waliojitokeza kujiandikiasha na darasa la kwanza kwa mwaka 2018
Mkuu wa Mkoa akiwasili katika shule ya msingi Mbande akiongozana na baadhi ya viongozi mbalimbali alioambatana nao katika hafla hiyo
Baadhi ya wakazi wa Mbande pamoja na wanachama wa Chama Chamapinduzi walijitokeza katika hafla hiyo
Wanafunzi wa darasa la kwanza wakiwa katika hafla hiyo
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akiwaaga wanafunzi wa shule ya msingi Maji Matitu iliyopo mbagala
Wananchi wa Mbande wakisindikiza gari  ya Mkuu wa Mkoa kwa furaha baada yakumaliza ziara yake shuleni hapo.




Mkuu Wa Wilaya ya Temeke Félix Lyaniva (kulia) akizungumza na wanafunzi pamoja na walimu 

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda amewataka wakuu wote wa Idara mbalimbali hususani katika sekta ya Elimu kutekeleza majukumu yao ili kuweza kutatua changamoto mbalimbali  za wananchi.

Rc Makonda ameyasema hayo leo alipofanya Ziara katika shule ya msingi Majimatitu na Shule ya Msingi Mbande zilizopo katika Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salam na kuangalia mpango mkakati wa halmashauri hiyo katika kutatua changamoto zilizopo katika shule hizo ambapo wanafunzi walioandikishwa kwa mwaka 2018 idadi imekuwa kubwa na kupelekea uhaba wa miundombinu katika shule hizo. 

Amesema ni wakati kwa wakuu wa idara katika sekta ya Elimu kutatua changamoto zilizopo katika sekta ya Elimu ili kusaidia elimu inakuwa kwa kiwango kikubwa na kutengeneza kizazi cha wasomi kwani elimu ni chachu ya maendeleo katika Jamii.

"Wakuu wa idara yapasa kuamka na kuweza kufuatilia kwa Mkurugenzi wako na kuweza kuatatua changamoto zote zilizopo katika idara yako nisisikie Mkuu wa Idara anasema nimeshindwa kutekeleza huu ni wito Wangu kwenu wakuu wote wa Idara zote katika Mkoa wangu"Amesema Rc Makonda. 

Aidha Makonda ametoa wiki mbili kwa Mkurugenzi wa manispaa hiyo pamoja na Mkuu wa Wilaya kuhakikisha wanatafta eneo la kuweza kujenga shule nyingine ambapo amesema baada ya kupatikana eneo hilo Ujenzi wa shule nyingine ya Mbande itakayosaidia kutatua changamoto ya idadi kubwa ya wanafunzi katika shule hiyo.

"Natoa wiki mbili kwa Mkurugenzi   pamoja na Mkuu wa Wilaya kuhakikisha eneo linapatikana la kujenga shule nyingine ya Mbande na mimi mwenyewe nitakuja kujenga msingi kabla ya tarehe 10 mwezi ujao niwe nimepata taarifa ya eneo hilo kupatikana ili tujenge shule nyingine"Amesema Makonda.

Katika shule ya Msingi Majimatiti wanafunzi walioandikishwa darasa la kwanza ni 976 ambapo idadi ni kubwa na katika shule ya Mbande pia idadi ya wanfunzi walioandikishwa kwa mwaka huu ni kubwa kuliko shule zote za Mkoa huo, ambapo wanafunzi walioandikishwa ni 1,132 n'a bado uandikishaji unaendelea hadi March 30 mwaka huu. 

Amesema halmashauri zinapaswa kuaandaa mpango mkakati wa muda mrefu wa za kuratatua changamoto hizo kwa kujenga shule pamoja na vyumba vya madarasa ili kusaidia n'a kuhakikisha changamoto kama hizi hazijitokezi tena na kuweza kuboresha sekta ya Elimu na kutengeneza kizazi kilicho bora chenye kuleta maendeleo katika jamii na taifa kwa ujumla. 


Akitoa taarifa ya jumla  ya Wilaya kielimu kwa mkuu wa Mkoa kaimu Afisa Elimu  msingi   wilaya ya Temeke Slyvia  Mutasingwa amesema manispaa hiyo inajumla ya wanafunzi 1,6625 , wavulana 81,718    wasichana 84,387  na Walimu 3,018 Wanaume 554      Wanawake 26,032   na kusema kuwa  Manispaa hiyo inaupungufu wa vyumba vya  Madarasa 1,565  huku mahitaji halisi yakiwa ni 3,718 na kufanya kuwa na upungufu vyumba 2149 na upungufu wa matundu vya vyoo 2,219 kwa  Mbande pekee  kuna mahitaji ya madarasa 153 madarasa yaliyopo ni  38  kunaupugufu wa madarasa 115,  kwa upande wa matundu ya choo kuna matundu 40 huku mahitaji halisi yakiwa ni 310, na kuna madawati 2298 yalipo ni 1990 kuna upungufu wa  madawati 308.




No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages