Mwanasheria
Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju na Mwenyekiti wa Baraza la
Wafanyakazi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu akimkaribisha Mhe Waziri wa
Katiba na Sheria kuzindua Baraza la Wafanyakazi na katika salamu zake
alisema ni muhumu kwa Serikali kuendelea kuiimarisha Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu kutokana na umuhimu wake katika maendeleo ya nchi,
kiuchumi, kiusalama, katika utawala wa sheria na katiba
Waziri
wa Katiba na Sheria Mhe. Profesa Paramagamba Kabudi akitabasamu mara
baada ya kufungua Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa
Serikali siku ya jumatatu. Baraza hilo linakutana kwa siku mbili katika
ukumbi wa LAPF mkoani Dodoma.
Wajumbe
wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali
wakiimba wimbo wa mshikamano wakati wa ufunguzi wa Baraza hilo, wajumbe
wa Baraza ni pamoja na Mawakili Wafawidhi wa Serikali, Wakuu wa
Divisheni na Vitengo, Wajumbe wa TUGHE na mada mbalimbali zilitolewa
wakati wa uzinduzi hao.
Mwanasheria
Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju amesema, kutokana na mchango
mkubwa wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu katika maendeleo ya kiuchumi,
usalama, utawala wa sheria na utawala bora, Kuna umuhimu wa Serikali
kuendelea kuiimarisha Ofisi hiyo.
Ameyasema
hayo wakati akimkaribisha Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe Profesa
Palamagamba Kabudi kuzindua Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Uzinduzi wa baraza hilo umefanyika siku
ya jumatatu katika ukumbi wa mikutano wa Jengo la LAPF Mkoani Dodoma.
Uzinduzi
wa Baraza hilo, ulitanguliwa na uchaguzi wa Katibu na Katibu
Msaidizi. Zoezi la uchaguzi lilisimamiwa na Katibu Mkuu wa TUGHE Mkoa
wa Dodoma Bw. John Mchenya, Naibu Katibu Mkuu TUGHE Taifa Bi. Jane
Mbura na Afisa Kazi Bi. Razina Tuusa. Waliochaguliwa kwa
kura za Siri ni Wakili wa Serikali Mkuu Monica Mbono ambaye
anakuwa Katibu na Bw. Michael Masanja anakuwa Katibu msaidizi.
Mhe.
Masaju akiwa ni Mwenyekiti wa Baraza la wafanyakazi, ameyataja maeneo
ambayo Serikali inatakiwa kuendelea kuyaimarisha katika Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu ni pamoja na, Raslimali fedha, mafunzo, makazi salama
kwaajli ya mawakili wa serikali na miundombinu ya ofisi.
“Mhe.
Waziri, yapo masuala ya kisera ambayo
tunaomba Serikali inayashughulikie ipasavyo ili kuiwezesha Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa
ufanisi. Maeneo hayo ni kuajiri Mawakili wa Serikali na Watumishi wa
Kada zingine, kujenga majengo ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu katika
Ofisi za Wilaya na Mikoa ili kuokoa fedha inayotumika kulipia pango”.
Ameleza Mwanasheria Mkuu.
Kwa
upande wa mafunzo, Mwanasheria Mkuu, ameishauri
Serikali katika kuwajengea uwezo wa kitaalam Mawakili wa Serikali
na watumishi wenzao katika maeneo ya kipaumbele na kuimarisha maslahi
ya mawakili wa serikali na watumishi wote katika Ofisi
ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Pamoja
na kutaja changamoto mbalimbali ambazo Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa
Serikali imekuwa ikikabiliana nazo katika utekelezaji wa Majukumu yake.
Mwanasheria Mkuu ametaja mafanikio ambayo Ofisi imeyapata katika
utekelezaji wa majukumu yake.
Baadhi
ya mafanikio hayo ni pamoja na kuokoa fedha nyingi na kuingiza
serikalini mapato kupitia uendeshaji wa mashtaka na mashauri mbalimbali
mahakamani na katika mabaraza ya usuluhishi, ushiriki katika
majadiliano ya Mikataba na uhakiki wake na kudumisha utawala wa sheria
na utengamano nchini.
Mafanikio
mengine ni pamoja na kuingiza serikalini kiazi cha shilingi 1.039
Bilioni iliyotokana na faini baada ya serikali kushinda kesi 110
zinazohusiana na makosa chini ya sheria ya uhifadhi wa wanyamapori ya
mwaka 2009.
Mafanikio
mengine ni urejeshwaji wa mali zilizopatikana kwa njia ya
uhalifu ambapo kesi 10 zilitolewa uamuzi na mali zenye thamani ya
zaidi ya Bilioni 2 zilitaifishwa. Vile vile Serikali ilishinda
kesi 3 zinazohusiana na utakatishaji wa fedha haramu ambapo mbali na
watuhumiwa kutiwa hatiani kiasi cha fedha kipatacho shilingi milioni
29,439,452 kilitaifishwa.
Mwanasheria
Mkuu wa Serikali akifafanua zaidi mafanikio yanayotokana na majukumu
ya Ofisi yake kuwa ni yale yanayotokana na mashauri mawili
yanayohusu kuingiza nchini magari mawili ya kifahari yaliyotolewa
uamuzi kwa watuhumiwa kupatikana na hatia na magari hayo
ambayo thamani yake ni shilingi bilioni 1.7 yalitaifishwa kuwa mali ya
serikali na fidia ya shilingi milioni 200 kulipwa serikalini.
Akizindua Baraza
la wafanyakazi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, Waziri wa Katiba na
Sheria, Mhe.Profesa Palamagamba Kabudi alipongeza uamuzi wa Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu kuzindua Baraza lake na kukutana kwa siku mbili
kujadili masuala mbalimbali.
Kwa
mujibu wa Waziri Kabudi, Baraza la Wafanyakazi ni chombo cha
kupanga mipango muhimu na kuhakikisha kuwa kinafanyika pia katika
kutathmini ambacho Ofisi imepanga kukifanya na kimefanyika kwa
kiwango gani.
Akasema
“sote tu mashahidi kuwa tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie
madarakani msisitizo umekuwa kwa kila taasisi kuongeza ufanisi katika
kutekeleza majukumu yake. Awamu hii inasisitiza watumishi na taasisi
kuondokana na tabia ya kufanya kazi kwa mazoea na kuhakikisha utendaji
wao unaleta tija katika serikali” ameeleza Waziri
Na
akalitaka Baraza hilo la wafanyakazi kutathimini ni jinsi
gani linaishauri serikali na taasisi zake katika masuala yote kwa
kuhakikisha kwamba ushauri unaotolewa unabeba maslahi mapaba ya taifa na
kuzingatia vipaumbele vya serikali ya awamu ya tano
Akasisitiza
pia kwamba tathmini hiyo inatakiwa kwenda mbali zaidi kwa kujiuliza
kama m Miswada inayoadaliwa inakidhi vigezo vya kitaalam, je inabeba
maslahi mapana ya nchi, au je jukumu la kuiwakilisha Serikali mahakamani
liinatekelezwa kwa kiwango gani cha ufanini, je kesi na mashauri yote
yanasimamiwa na kuendeshwa kwa weledi na uzalendo na ni kwa kiasi gani
uratibu wa upelepezi na uendeshaji wa mashauri unafanyika kwa weledi na
umakini.
Baraza
la Wafanyakazi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali linahudhuriwa
na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni Mwenyekiti wa
Baraza, naibu Mwanasheria Mkuu, Bw. Gerson Mdemu ambaye pia ni Makamu
Mwenyekiti , Mkurugenzi wa Mashtaka, Bw. Biswalo Maganga,
Mawakili Wafadhiwi kutoka Mikoa yote na Wilaya ambako kuna Ofisi za
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Wakuu wa Divisheni na Vitengo na Na
wajumbe wa TUGHE.
Aidha mada mbalimbali zinatolewa zikiwamo zinazohusu maadili katika utumishi wa umma na utunzaji wa siri za serikali.
No comments:
Post a Comment