A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, December 6, 2017

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa DSM Kitengo cha Afya yapokea hundi ya shilingi milioni kumi kutoka Kampuni ya CNBM


Katika  kuunga Mkono juhudi zinazofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaamPaul Makonda  kusaidia Watu wenye uhitaji wa miguu bandia na zoezi la upimaji afya,Kampuni ya China Nationali building Material Group leo imekabidhi hundi ya Shilingi Milioni kumi.
Akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya kupokea msaada huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Dakta Grace Magembe amesema Serikali ya Mkoa imekusudia kutatua changamoto za kiafya kwa wananchi pamoja na kusaida watu wenye ulemavu,ambapo amebainisha kuwa hapo awali Serikali ya Mkoa ilikusudia kusaidia watu wenye ulemavu miambili lakini idadi ya wenye uhitaji wa miguu ni zaidi ya watu elfu moja hivyo amewataka wadau kuendelea kujitokeza kusaidia.

Dakta Magembe ameongeza kuwa tokea kuingia madarakani Serikali ya awamu ya tano ilio chini ya Rais Dakta John Magufuli imekuwa ikishughulikia changamoto mbalimbali za wananchi hivyo amewataka wananchi kuendelea kuunga mkono juhudi hizo.
Kwa upande wake Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya China National building Material Group  Wang Shupeng amesema kampuni hiyo imeridhishwa na juhudi zinazofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam na imetambua umuhimu wa kusaidia watu wenye mahitaji maalumu ikiwemo miguu bandia hivyo mbali na msaada huo wa shilingi milioni  kumi za kitanzania itaendelea kutoa misaada mbalimbali kwa Serikali.
Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages