Rais wa Marekani Donald Trump amemuambia
waziri wake wa mashauri ya nchi za nje kuwa anatupa muda wake akijaribu
kufanya mazungumzo na Korea Kaskazini kuhusu mpango wake wa nyuklia.
"Jiwekee nguvu zako Rex, tutafanya kile
kitahitajika kufanywa," Bw. Trump aliandika kwenye twitter baada ya
kuibuka madai kuwa Marekani ilikuwa kwenye mazungumzo na Pyongyan.
Rex alifichua hayo siku ya Jumamosi akisema kuwa Korea Kaskazini haitili maanani mazungumzo hayo.
Nchi hizo mbili zimekuwa kwenye majibizano makali miezi ya hivi karibuni.
Marekani inataka Korea Kaskazini
kusitisha mipango yake ya silaha baada ya kufanya majaribio kadha ya
makombora ya na kudai kufanya jaribo la bomu la haidrojeni ambalo
linaweza kutundikwa kwa kombora la masafa marefu.
Hi sio mara ya kwanza Donald Trump amekinzana na maafisa wa vyeo vya juu kwenye utawala wake.
Mwezi Agosti alisema kuwa jeshi la
Marenia lilikuwa tayari kukabiliana na Korea Kaskazini, saa chache baada
ya waziri wake wa ulinzi kujaribu kutuliza misukosuko akisema kuwa
jitihada za mazungumzo zilikuwa zinafanikiwa.
Matamshi yake yanakuja siku moja bada ya
Bw Tillerson kufichua kuwa maafisa wa Marekani walikuwa na mawasiliano
na Korea Kaskazini licha na kuwepo vita vya maneno kati ya viongozi wa
nchi hizo mbili.
No comments:
Post a Comment