A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, September 9, 2017

RC MAKONDA AWEKA JIWE MSINGI LAUJENZI WA KARAKANA YA JIJI LA DAR ES SALAAM.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es`Salaam Paul Makonda akikata utepe kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa viwanda vidogo vidogo katika karakana ya jiji la Dar es Salaam iliyopo Mwananyamala leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya majengo ya mradi wa viwanda vidogo vidogo katika karakana ya jiji iliyopo Mwananyamala jijini Dar es Salaam.
Balozi wa China ,Dk. Lu Youqing akipiga mpira katika uwanja bandari wakati makabidhiano ya uwanja huo na Mkuu wa Dar es Salaam, Paul Makonda. 
Monekano wa Uwanja wa Bandari uliokarabatiwa na Ubalozi wa China leo jijini Dar es Salaam.
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amezitaka Manispaa zote za Mkoa wa Dar es Salaam zitengeneze mazingira rafiki kwa wajasiriamali wadogo ili kuwawezesha na fursa mbalimbali za biashara . 

Makonda ameyasema hayo leo wakati wa kuweka jiwe la msingi katika uzinduzi wa viwanda vidogovidogo katika Karakana ya Jiji iliyopo Mwananyamala Jijini Dar es Salaam, amesema kuweka mazingira rafiki ya viwanda kutasaidia wajasiriamali kujitokeza na kuyatumia na nchi kuweza kupata maendeleo pamoja na kukuza uchumi wa kufikia uchumi wa kati. 

"Niwapongeze kwa kazi mnayoifanya kwa manispaa lakini pia kuunga mkono jitihada za wajasiriamali kwa kuwapa mikopo kupitia vikundi vyao na nitoe wito pia kwa watendaji msitoe mikopo holela itakuwa kazi kuzirejesha" Amesema RC Makonda. 

Aidha amesema kuwa Halmashauri ya Jiji imejenga mazingira rafiki kwa kuanza kutoa Ruzuku kwa manispaa ambapo ilikuwa hafanyi hivyo katika miaka iliyopopita.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam,Sipora ya Liana amesema kuwa kupitia mradi huo Jiji la Dar es Salaam limeendelea kutoa kipaumbele kwa wanawake, vijana na walemavu wanaopata mikopo kutoka Halmashauri ya Jiji kwa kuona mazingira wanayofanyia kazi sio rafiki na wanahangaika sana kupata masoko.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages