Kijiweni Production Kuonyesha Filamu Agosti 11 mwaka huu, filamu iitwayo
‘T-Junction’ itaonyeshwa kwenye jumba la sinema lililoko Mlimani City
jijini Dar. Habari hiyo imesemwa na kuthibitishwa na kampuni ya
Kijiweni Production.
habari kamili kuhusu Kijiweni Production Kuonyesha Filamu
Akizungumza na wanahabari jijini Dar leo, Mwongozaji Mkuu wa Filamu hiyo,
Amil Shivji, amesema kuwa filamu hiyo baada ya kuonyeshwa siku hiyo
itaendelea kuchezwa hapa nchini na duniani kote kwani imechaguliwa pia
kuwa mojawapo ya filamu za juu za Afrika ambazo zitaonyeshwa katika
matamasha ya filamu nyingi Ulaya.
“Kuhusu T-Junction, ni filamu inayowahusu mabinti na jamii zao, jamii
moja ikiishi kiholela. Faraja yao ni kujua wana umoja na furaha. Jamii
yao inazingatia mifumo, kanuni na taratibu za utu,” alisema Shivji.
Tukio la Kijiweni Production Kuonyesha Filamu litafanyika jijini Dar es
Salamam baada ya kuonyeshwa kwenye Tamasha la ZIF lililofanyika
Stonetown, Zanzibar, hivi karibuni.
No comments:
Post a Comment