A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, November 23, 2021

Benki Ya Exim Yakabidhi Msaada Wa Madawati 100 Kwa Ajili Ya Mkoa Wa Mwanza

 


Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel (katikati) sambamba na viongozi waandamizi wa benki ya Exim akiwemo Mkuu wa Idara ya Rasimimali watu wa benki hiyo Bw Fredrick Kanga (Kulia- walioketi) na Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano kutoka Benki ya Exim, Stanley Kafu (kushoto- walioketi) wakiwa wameketi katika moja ya madawati 100 yaliyotolewa na benki ya Exim Tanzania kwa ajili ya Mkoa wa Mwanza yakiwa ni sehemu kampeni ya ugawaji madawati 1000 yaliyofadhiliwa na benki hiyo kwa ajili ya shule za msingi katika mikoa mbalimbali nchini. Wengine ni maofisa waandamizi wa elimi kutoka mkoa huo.


Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel (Kulia) akipokea msaada wa madawati 100 kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano kutoka Benki ya Exim, Stanley Kafu (kushoto) kwa ajili ya kusaidia kuondoa adha ya upungufu wa mawadati katika Shule mbalimbali za Msingi mkoani Mwanza ikiwa ni sehemu ya mpango wa benki hiyo wa ugawaji wa madawati 1000 katika mikoa mbalimbalimbali hapa nchini kupitia mpango wake wa kusaidia jamii ujulikanao kama Exim Cares.


Sehemu ya madawati 100 yaliyotolewa na benki ya Exim Tanzania kwa ajili ya Mkoa wa Mwanza yakiwa ni sehemu kampeni ya ugawaji madawati 1000 yaliyofadhiliwa na benki hiyo kwa ajili ya shule za msingi katika mikoa mbalimbali nchini.


Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel (kushoto) akijipongeza na Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Bi Veronica Kessy wakati wa hafla ya makabidhiano madawati 100 yaliyotolewa na benki ya Exim Tanzania kwa ajili ya Mkoa wa Mwanza yakiwa ni sehemu kampeni ya ugawaji madawati 1000 yaliyofadhiliwa na benki hiyo kwa ajili ya shule za msingi katika mikoa mbalimbali nchini.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages