A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, May 12, 2018

Serikali yakanusha Taarifa za UONGO Kuhusu Bodi ya Mikopo

Serikali ya kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imefunguka na kukanusha taarifa zinazosambazwa katika mitandao ya kijamii kuwa wanafunzi ambao wazazi wao wana leseni za biashara hawataruhusiwa kupata mkopo wa elimu kuwa sio za kweli na kuutaka uuma kuzipuuza taarifa hizo.

Kauli hiyo imetolewa leo Mei 11, 2018 na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mh. William Ole-Nasha wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kufuatia taarifa zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na hoja za baadhi ya Wabunge walizotoa bungeni kuwa leseni ya biashara inatumika kama kigezo cha kutowapa wanafunzi mikopo hiyo.

"Hizo habari ni za uongo zenye lengo la kupotosha jamii, kimsingi tuna taka umma wa watanzania wazipuuzie hizo taarifa kwasababu sio za kweli. Mikopo inatolewa kwa kuzingatiwa uwezo wa mzazi au mlezi wa mwanafunzi, kwa hiyo kinachoangaliwa ni kipato chake", amesema Ole-Nasha.

Pamoja na hayo, Naibu Waziri Ole-Nasha ameendelea kwa kusema "vigezo vinavyotumika vinabadilika kila mwaka kulingana na maboresho yanayofanywa ili kuendana na wakati ambapo kwa mwaka huu mabadiliko hayo yamesaidia kuongeza wanufaika wa mikopo elfu 10,000 zaidi kulinganisha na mwaka jana.

Kwa upande mwingine, Naibu Waziri iza, Mh. William Ole-Nasha amesema mwaka huu matarajio ni kutoa mkopo kwa wanafunzi laki moja na elfu ishirini na mbili (122,000) na kati yao elfu 30 ni wa mwaka wa kwanza na elfu 80 ni wanafunzi wanaoendelea na masomo yao.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages